• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AKABIDHI MSAADA WA CHAKULA KWA KAYA ZILIZOATHIRIKA NA MVUA KUBWA YA 23, MACHI, 2023

Posted on: May 9th, 2023

Na. Elinipa Lupembe.


Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, amekabidhi jumla ya tani 4.4 za mahindi na Kilo 290 za maharage kwa kaya 323 ziliathirika zaidi kutokana na mvua kubwa, zoezi lililofanyika kwenye ofisi ya kata ya Olturumet.


Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo wa chakula, mkuu huyo wa wilaya, licha ya kutoa pole nyingi kwa wananchi,amewataka, kuendelea kushikamana na kusaidiana panapotokea matatizo katika maeneo yanayotuzunguka.


Amesema kuwa, serikali inatambua madhara yaliyoyapata wananchi, licha ya msaada huo mdogo wa chakula, iko kazini kuendelea kufanya marekebisho ya miundombinu ya barabara kupitia TARURA pamoja na kutumia mitambo ya halmashauri.


Aidha amewataka wananchi kuchukua tahadhari kubwa wakati wa mvua, huku wakiendelea kutunza mazingira, na kuwakemea watu wote wanaoharibu mazingira, kwa kuwa uharibifu huo ndio unasababisha madhara haya mvua zinaponyesha.


"Historia inaonyeshwa kwa kuthibitihsiwa na wazee wa maeneo haya, kuwa zamani mvua zilinyesha kubwa zaidi lakini kutokana na uharibifu wa mazingira kwa sasa mvua ndogo inaleta madhara makubwa sana, wazee wametuomba kuchukua hatua ili kuzuia, madhara haya yasiendele kutokea miaka ijayo, tunaendelea kuchunguza tutachukua hatua". Amesisitiza Mhe. Emmanuela


Amewasihi, watu wote waliojenga na kufanya shughuli za kilimo kwenye miinuko, vilima na vyanzo vya maji, waache mara moja, wasipofanya hivyo Serikali itawaondoa kwa nguvu.


Hata hivyo, viongozi wawakili wa wananchi, wakiwemo waheshimiwa wenyeviti wa vijiji na vitongoji na Madiwani, wameishukuru serikalipitia ofisi ya mkuu wa wilaya kwa msaada huo wa chakula, msaada ambao ni muhimu kwa wananchi hao waliopata madhara yaliyotokana na mvua kubwa.


 "Tunakushukuru Mheshimiwa mkuu wa wilaya, tangu siku ya kwanza mafuriko yalipotokea, hukutuacha umekuwa pamoja nasi na umeenda mbali zaidi kwa kuwaletea wananchi hawa chakula, ambacho wengi wao akiba yao ya chakula ilichukuliwa na kuharibiwa na mvua hizo" Wamesema Viongozi hao


Hata hivyo viongozi hao wawakilishi wa wananchi, wameiomba serikali, kuweka mpango wa madhubuti wa kurekebisha barabara ambazo zimeharibiwa na mvua, barabara nyingi hazipitiki, na kusababisha adha kubwa kwa wananchi katika maeneo mengi.


"Tunashukuru kwa juhudi za serika, kutoa mitambo kuzibua mitaro, tunaiomba serikali, kuongeza nguvu katika  kutengenezewa barabara, baadhi ya maeneo hayapitiki na kusababisha mateso makubwa kwa wananchi" Amesisitiza Diwani kata ya Olturumet, Mhe. Joseph Tinayo.


Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi, licha ya kutoa pole kwa wananchi hao, amefafanua kuwa kati ya mahindi tani hizo 4.4, Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini imetoa Kilo 3,000 za mahindi na Kilo 290 za maharage huku Serikali kupitia Ofisi ya Mkuu wa wilaya imetoa jumla ya Kilo 1,400, madaftari 300 na kalamu 336 kwa wanafunzi 188.


Awali jumla ya kaya 543 zilipata madhara  kutokana na mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia tarehe 23 mwezi Machi, 2023, huku kaya 323 ziliathirika zaidi ndizo zilizopewa msaada wa chakula kutoka kata za Kimnyaki, Sambasha, Olturumet, Olmotony na Oloirieni.


ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.