• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AMEWATAKA WANANCHI KUUENZI MUUNGANO KWA KUSHIRIKIANA KULIJENGA TAIFA LA TANZANIA

Posted on: April 20th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Emanuela Kaganda, amewataka wakazi wa halmashauri ya Arusha, kuuenzi, kuulinda na kuutetea Muungano  kwa kushirikiana kufanya kazi kwa bidii juhudi na maarifa ili kuendelea kutunza na kuimarisha tunu za Muungano.

Mhe. Emmanuel, ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa wiki ya maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano, uzinduzi uliofanyika kwenye shule ya sekondari Mringa kata ya Oloirieni, halmashauri ya Arusha.

"Leo tunazindua rasmi wiki ya Maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano tangu nchi za Tanganyika na Zanzibar kuungana, Muungano ambao umebebwa na misingi ya Uhuru na Umoja, tunapaswa kufahamu kuwa misingi hiyo ndiyo nguzo ya Taifa letu la Tanzania na wananchi wa pande zote mbili". Amefafanua Mkuu huyo wa wilaya.

Mh. Emmanuela amewasisitiza wananchi wa Wilaya ya Arumeru kuutetea, kuupigania, kuusimamia na kuulinda Muunga kwa nguvu zote, sambamba na kutoa elimu sahihi kwa wananchi wengine ambao hawana taarifa sahihi kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

"Ndugu zangu tusimame kkidete, tusimame imara kuutetea, kuupigania, kuusimamia na kutoa elimu sahihi kwa wananchi wengine ambao hawaufahamu vizuri Mmuungan, tuwafundishe watoto wetu kuhusu Muungano na tunu zake, someni na shirikini kwenye midahalo inasaidia kupata maarifa na kkutjenga kupitia taarifa mbalimbali zinazotolewa kwenye vyombo vya habari kwa manufaa ya nchi yetu". Amesisitiza Mkuu huyo wa wilaya.

Aidha amewapongeza waasisi wa Muungano Hayati Mzee Abeid Karume na Mwl. Julius Kambarage Nyerere kwa maamuzi yayaya busara na muhimu kwa watanzania kwa kuunganisha nguvu, kwa kuwa Umoja ni nguvu na uengano ni udhaifu.

Amezitaja Sababu za msingi za kuungana Tanganyika na Zanzibar, ni ukaribu wa nchi hizi mbili uliosababisha muingiliano wa kijamii, udugu wa damu kati ya wananchi nchi hizi mbili, pamoja na mwingiliano wa kibiashara pamoja na urafiki, undugu na uongozi wa pande zote mbili.

Hata hivyo ameweka wazi kuwa Muungano huu, umeongeza wigo kwa wananchi wa pande zote mbili kuendelea kutumia kutumia fursa zinazopatikana kati ya Tanzania Bara na Visiwani, fursa amamba licha ya kudumisha udugu, zina lengo la kuleta maendeleo kwa watanzania wa pande zote.

"Tunayashuhudia, matunda ya Muungano yanayoyojengwa kwenye misingi ya uhuru na umoja, iliyobeba dhana kubwa ya  upendo, amani  na mshikamano wenye dhana ya udugu wa enzi na enzi, niwatake ndugu zangu, kila mmoja kusimamia misingi ya Muungano kwa kuutunza, kuulinda na kuenzi mambo yote mema kwa manufaa ya watanzania wote kwa ujumla wake". Amefafanua Mkuu huyo wa wilaya

Kauli mbiu ya Muungano 2023: "Umoja na mshikamano ndio nguzo ya kukuza uchumi wetu"


PPCHA ZA MATUKIO




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.