• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AWAAGIZA TANROAD, TARURA NA VIONGOZI WWNGINE KUSHIRIKIANA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA MVUA ZA EL NINO....

Posted on: October 2nd, 2023


Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda amewaagiza TANROAD, TARURA pamoja viongozi wengine ndani ya Wilaya ya Arumeru kushirikiana kuchukua tahadhari dhidi ya Mvua za El Nino zinazotarajiwa kunyesha hivi karibuni kwa kurekebisha mitaro inayoelekeza maji kwenye makazi ya watu.


Mhe. Emmanuela amesema hayo wakati akikagua miundombinu ya ujenzi wa barabara ya mianzini, Olemringaringa, timbolo - Ngaramtoni ambapo ambapo amewaagiza TANROAD kushughulikia changamoto za wananchi wanaoishi pembezoni mwa barabara hiyo ikiwemo kuwajengulea vivuko vya kuingilia kwao.


"TANROADS warekebishe maeneo ya njia ambazo wananchi wanatakiwa kupita pamoja na njia ndogo ndogo ambazo zinaunganisha barabara hiyo ya lami lakini pia kutengeneza makinga mvua ambayo yatapunguza kasi ya maji kwenda kwenye makazi ya watu ili mvua hizo zisilete madhara kwa wananchi". Ameagiza Mkuu huyo wa Wilaya.


Hata hivyo, ametoa rai kwa wananchi wote wanaoishi kwenye njia za mikondo ya asili ya maji kuanza taratibu za kuhama maeneo hayo ili kuepusha madhara yatakayoweza kujitokeza na kuongeza kuwa, wilaya ya Arumeru imejipanga vyema kuhakikisha kuwa wanakabiliana na mvua hizo ili madhara yaliyotokea wakati wa kipindi cha mvua zilizonyesha mwezi April yasitokee tena.


Aidha, madiwani kutoka kwenye Kata zilizoathirika na mafuriko ya mvua za masika za mwaka huu wamejitokeza kwa pamoja kujadili namna ya kudhibiti janga hilo kwa kutafta njia bora za kuchepusha maji yanayopita kwenye barabara hiyo kwenye mito iliyokaribu pamoja na kutengeneza makinga mvua kwenye eneo la kitako cha mlima Meru, msitu wa chuo cha Olmotonyi kwani kutokana na ujenzi wa miundombinu ya barabara hiyo inachochea maji kuongezeka na kuelekea kwenye makazi ya wananchi.


"Ujenzi wa barabara hii ni muhimu sana na yenye manufaa kwa wananchi wa Kata hizi hasa akina mama kwani itawarahisishia kufanya shughuli zao za mendeleo ya kiuchumi kutokana na kuwepo kwa usafiri wakati wote, lakini ni vyema kuangalia uwepo wa barabara hii isiwe kero kwa miundombinu yake kuelekeza maji kwenye makazi yao na kusababisha mafuriko". Amesema Diwani wa kata ya Sambasha.


Naye kiongozi wa Mila kijiji cha Timbolo, Laigwanan Raleto Raphael amesema kuwa ni vyema TANROADS kushirikiana na wananchi wakazi wa maeneo hayo kurekebisha maeneo yote mapema ili wananchi waweze kupita kirahisi na kuendelea na shughuli zao za kila siku kabla ya mkandarasi kuondoka kwenye eneo la kazi.


Hata hivyo, Mhandisi wa TANROADS, Hophine Mollel ameahidi kufanyia kazi changamoto zote zilizowasilishwa na wananchi wa kata hizo kwa wakati kabla ya ya mvua hizo kuanza kunyesha.


Awali, wananchi hao waliwasilisha changamoto hizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Arumeru kutokana na ujenzi wa makarvati ya barabara hiyo kuelekeza maji kwenye makazi yao hali ambayo ingeweza kusababisha mafuriko wakati wa mvua.


UJENZI WA BARABARA UENDANE NA MIUNDOMBINU YA MAJI KUZUIA ATHARI ZA MVUA




Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.