• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AWASISITIZA MADIWANI ARUSHA DC, KUIMARISHA MIKAKATI YA UKUSANYAJI WA MAPATO

Posted on: November 6th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango, ametoa salamu kwa wajumbe wa baraza la Madiwani kwa kuushukuru na kuupongeza uongozi wa halmashauri ya Arusha kwa juhudi kubwa zinazofanyika katika kuwahudumia wananchi na kuwasisitiza kuimarisha mikakati ya ukusanyaji wa Mapato.

Akizungumza baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la kujadili taarifa za robo ya kwanza cha Julai -Septemba 2022, Mkuu huyo wa wilaya, amewahimiza waheshimiwa Madiwani licha ya juhudi zinazofanyika suala la ukusanyaji wa mapato ni la muhimu zaidi pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Mkuu huyo wa wilaya ameweka wazi kuwa, ili halmashauri iweze kutimiza mipango na malengo yake, ni lazima ukusanyaji wa mapato ufanyike kwa ufanisi kulingana na makisio ya kibajeti pamoja na kusimamia matumizi ya mapato hayo.

Aidha mhandisi Ruyango, amesisitiza matumizi ya makusanyo yanayozingatia sheria na maelekezo ya serikali ikiwemo asilimia 10 za kwa ajili ya mikopo isiyokuwa na riba kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kama maelekezo ya serikali yanavyoelekeza.

Hata hivyo, mkuu wa wilaya amemsisitiza mkurugenzi wa halmashauri hiyo, kusimamia makusanyo ya mapato hasa kwa mapato yanayokusanywa kwa mashine za POSS kuweka fedha hizo benki kama sheria inaelekeza ya kuwasilisha fedha zote benki mara baada aya kuzikusanya.

Awali amewakumbusha waheshimiwa madiwani, kushiriki katika usimamizi wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao, pamoja na kuwashirikisha wananchi katika usimamizi wa miradi hiyo.

"Halmashauri imepokea fedha kutoka Serikali Kuu,  shilingi milioni 760 za ujenzi wa vyumba 38 vya madarasa kwa shule 15 za sekondari kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka wa masomo 2023, hivyo kila aliyepewa dhamana ahakikishe anashiriki kikamilifu kusimamia miradi hiyo kwa mujibu wa sheria".Amesisitiza Mkuu wa wilaya .

Aidha amaemuagiza Mkurugenzi wa halmashauri kutoa taarifa kwa viongozi wa ngazi zote ikiwemo Madiwani, za miradi yote inaokwenda kutekelezwa  kwenye maeneo yao ya kata, vijiji na vitongoji, ili viongozi wote washiriki katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Waheshimiwa Madiwani, mnatakiwa kufanya mipango ya kuhamasisha wanafunzi wanapata chakula cha mchana wawapo shuleni na kuwahasisha wazazi kuchangia changia chakula cha mchana kwa shule za kutwa.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍


Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango akizungumza kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani, halmashauri ya Arusha wa kujadili taarifa za robo ya kwanza ya Julai - Septemba 2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.


Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, Mhe. Ojung'u Salekwa akifungua Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kujadili taarifa za robo ya kwanza ya Julai - Septemba 2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.


Baadhi Madiwani wakiwa kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kujadili taarifa za robo ya kwanza ya Julai - Septemba 2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.


Baadhi Madiwani wakiwa kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kujadili taarifa za robo ya kwanza ya Julai - Septemba 2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.


Baadhi Wakuu wa Idara na Vitengo, halmashauri ya Arusha wakiwa kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kujadili taarifa za robo ya kwanza ya Julai - Septemba 2022, mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.