Na Elinipa Lupembe
Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, amewataka walimu kuanza mwaka wa masomo 2023, kwa kuongeza bidii na maarifa zaidi katika kufanya kazi ili kuhakikisha wanafunzi wanafundishwa na hatimaye kufanya vizuri kwenye masomo yao kama ilivyokuwa mwaka uliopita wa 2022.
Mheshimwa Ruyango amesema hayo wakati akitoa salamu za mwaka mpya alipokutana na watalamu wa idara za elimu msingi na sekondari, halmashauri ya Arusha wakiwemo wakuu wa shule za sekondari, walimu wakuu wa shule za msingi pamoja na Maafisa Elimu kata, kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.
Mkuu huyo wa wilaya licha ya kuwapongeza walimu kwa kufanya kazi nzuri mwaka 2022, kazi ambayo tayari matokeo ya mitihani ya kitaifa yametoa tathmini ya utumishi ulio bora kwa walimu, wanafunzi, wazazi na wadau wa elimu wilaya ya Arumeru.
"Ninatambua kazi kubwa mliyoifanya walimu mwaka 2022, tumepambana kwa umoja wetu, kuhakikisha wanafunzi wamefundishwa na kuweza kufanya vizuri mitihani yao ya ndani na ile ya Taifa na kumaliza mwaka salama, ninawapongeza sana na niwatake mwaka 2023 kwa pamoja tuongeze bidii zaidi". Ameweka wazi Mkuu huyo wa wilaya.
Amesisitiza kuwa, walimu wana dhamana kubwa ya maisha ya watu, kwa kuwa mwalimu ndio kiwanda cha kuzalisha watalamu wote duniani, na kuwataka kutumia dhamana hiyo kuzalisha watalamu ambao ndio wajenzi wa Taifa hili.
"Shule zinafunguliwa Jumatatu ya tarehe 09, Januari 2023, hakikisheni wanafunzi wote wanaotakiwa kuwa shuleni wamefika na kuanza masomo mara moja, wanafunzi waliopangiwa kuajiunga na kidato cha kwanza walimu hakikisheni wameripoti shuleni kwa idadi yao, kama kuna changamoto yoyote toeni taarifa ili iweze kupatiwa ufumbuzi mapema". Amesema Mhandisi Ruyango
Aidha ameutaka uongozi wa halmashauri licha ya kusimamia ufanyaji kazi wa watumishi, usimamizi huo uende sambamaba na kusimamia maslahi ya watumishi kwa kuhakikisha kila mtumishi anapata haki zake za kisheria kama miongozo ya utumishi inavyoelekeza, jambo litakalomfanya mtumishi kuwa na moyo wa kutekeleza majumu yake.
Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, amekiri kupokea maelekezo hayo na kuyafanyia kazi kulingana na taratibu za Utumishi wa Umna na kuongeza kuwa halmashauri inatambua na kuthamini kazi kubwa ya kuwahudumia wananchi inayofanywa na watumishi wa kada zote.
Hata hivyo walimu wamemshukuru na kumpongeza mkuu huyo wa wilaya, kwa kukutana na walimu na kuahidi kushirikiana kwa pamoja kufanya kazi kwa bidii zaidi na kuhakikisha wanafunzi wanapata ujuzi na maarifa utakao wawezesha kupandisha kiwango cha taaluma.
Aidha wameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongzwa na mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia shuleni ikiwe miundombinu ya madarasa, nyumba za walimu pamoja na vifaa vya kiditali vya kufundishia.
ARSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango akitoa salamu za Mwaka mpya kwa watalamu wa elimu msingi na sekondari wakiwemo wakuu wa shule za sekondari, Maafisa Elimu ngazi ya kata na halmashauri, Walimu Wakuu shule za masingi halmashauri ya Arusha, kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha akizungumza kwenye mkutano uliojumuisha watalamu wa elimu msingi na sekondari wakiwemo wakuu wa shule za sekondari, Maafisa Elimu ngazi ya kata na halmashauri, Walimu Wakuu shule za masingi halmashauri ya Arusha, kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.
Baadhi ya wakuu wa shule za sekondari, walimu wa wakuu shule za msingi na Maafisa Elimu kata wakiwa kwenye mkutano na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango, kwenye ukumbi wa mkutano halmashauri ya Arusha
Walimu wakuu wa shule za sekondari, walimu wakuu shule za msingi na Maafisa Elimu kata wakiwa kwenye mkutano na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhandisi Richard Ruyango, kwenye ukumbi wa mkutano halmashauri ya Arusha
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.