• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU AMETOA SIKU 14 KWA VIONGOZI WA VIJIJI VYA LOSINONI JUU NA KISIMIRI JUU KUANDAA MAPENDEKEZO YA MARIDHIANO ILI KUTATUA MGOGORO WA ENEO LA MALISHO.

Posted on: October 4th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, mheshimiwa Mhandisi Richard Ruyango, ametoa siku 14 viongozi wa vijiji vya Kisimiri Juu, kata la Uwiro halmashauri ya Meru na kijiji cha Losinoni Juu kata ya Oldonyowasi, halmashauri ya Arusha, kukaa vikao na kutoa mapendekezo ya maridhianao lengo likiwa kutatua mgogoro wa eneo la malisho katika mlima Lekishori, eneo linalogombewa na  wananchi wa pande hizo mbili.

Mkuu huyo wa wilaya ametoa siku 14 kwa viongozi hao, baada ya kukutana na wananchi wa vijiji hivyo viwili kwa nyakati tofauti huku kila upande ukionyesha hauna shida na upande mwingine, lakini kila upande ukilalamikia upande mwingine kuwa, ndio chanzo cha mgogoro huo, mgogoro unaohusisha eneo  la nyanda ya malisho, wanalodai  lililotengwa miaka mingi iliyopita na wazee wao, kwa ajili ya malisho ya mifugo.

Aidha mheshimiwa Ruyango, amefikia uamuzi huo, baada ya maelezo ya  viongozi wa pande zote mbili pamoja na wananchi wao kuweka wazi kuchoshwa na mgogoro huo, mgogoro ambao unawaumiza sana wananchi wa pande zote mbili, kwa kuwa unasababisha  kutokuelewana kwa muda mrefu, na kusababisha  watu kupoteza  mali zao na mtu mmoja kupoteza maisha, huku kila upande ukionyesha ari na matamanio ya kumalizika kwa mgogoro huo ili wananchi hao waweze kuishi kwa amani na utulivu kama ilivyokuwa hapo awali.

Viongozi waliotajwa kukutana na kuleta mapendekezo ya madhiano yao kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ndani ya siku hizo 14, ni pamoja na viongozi wawakilishi wa  wananchi wakiwemo wenyeviti wa vijiji vya Losinoni Juu na Kisimiri Juu, Waheshimiwa  Madiwani wa kata hizo mbili za Owiro na Oldonyowasi, maafisa watedaji wa vijiji na kata zote mbili, Maafisa Tarafa wa Tarafa hizo mbili pamoja na viongozi wa mila, maarufu kama Malaigwanani wa pande zote mbili.

"Nyinyi viongozi wa wananchi ninawapa siku 14, nendeni mkakae kila kila kijiji na viongozi wake, mkalete mapendekezo ya maridhiano ya nini kifanyike ili kumaliza mgogoro huo, makubaliano  hayo yawasilishwe kwenye yangu ndani ya siku hizoo 14, kwa ajili ya utekelezaji wa kukutanisha pande zote mbili, lengo letu kubwa ni kumaliza mgogoro huu, ili muendelee kuishi kwa amani na utulivu, kama  yalivyo matamanio yenu nyote mliyotuleza hapa kwenye mikutano" amesisitiza Mkuu wa Wilaya Ruyango.

Hata hivyo viongozi hao wa vijiji vyote viwili vinavyolumbana wamekiri mbele ya mkutano kuwa, wanahitaji kumalizika kwa mgogoro huo wa muda mrefu, mgogoro ambao wamekiri unarudisha nyuma maendeleo katika maeneo yao, kutokana na wananchi wao kutumia muda mwingi kwenye malumbano, badala ya kujikita kwenye mipango ya maendeo.

Viongozi hao licha ya kumpongeza mkuu huyo wa wilaya kwa kukutana nao na kufanya mikutano nao, mikutano iliyowapa fursa ya kutoa yao ya moyoni, huku wakionyesha uhalisia wa mgogoro huo, na kukubali kukaa kila upande na  kuandaa mapendekezo ya maridhiano ndani ya siku hizo 14 walizopewa, huku wakiomba kumalizika kwa mgogoro huo unaotesha wananchi wao.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kisimiri Juu, mheshimiwa Mbaiyani Kuresoi. amethibitisha kuwa maamuzi hayo ya mkuu wa wilaya yako sahihi na wao kama  viongozi wa wananchi wako tayari kufanyia kazi maagizo hayo, ili kumaliza kabisa tofauti zao, ambapo amekiri kuwa wananchi wa vijiji hivyo viwili kwa asili ni ndugu, hata kabla ya kugawanywa kwa mipaka ya halmashauri hizo mbili za Arusha na Meru.

Naye mwenyekiti wa kijiji cha Losinoni Juu, mheshimiwa Saitoti Ngoilenya, hakuwa tofauti na wananchi wengine, amekiri kutumia fursa hiyo waliyoipata kutoka kwa mkuu wao wa wilaya, kuandaa mapendekezo ya maridhiano ya eneo hilo la malisho, huku wakiweka mbele maslahi ya wananchi wa pande zote mbili, hasa amani na utulivu, unaosababisha kujikita kwenye shughuli za maendeleo na si migogoro tena.

"Tumechoshwa na mgogoro huu, unaokosesha amani wananchi wetu wa pande zote mbili, wananchi ambao kwa asili sisi ni ndugu moja, hatuoni haja ya kulumbana kwa ajili ya eneo ambalo limewekwa na Mungu, na tangu enzi babu zetu walilitunza na kulitumia kwa amani, maagizo ya mkuu wetu wa wilaya tunakwenda kuyafanyia kazi na tunaamini mgogoro huu sasa utafika mwisho " amesisitiza Mwenyekiti huyo wa Kijiji cha Losinoni Juu.

Awali mgogoro huo, uliodumu kwa  zaidi ya miaka mitatu sasa  tangu mwaka 2018, unaohusisha kijiji cha Kisimiri Juu kilichoko halmashauri ya Meru na Kijiji cha Losinoni Juu cha halmashauri ya Arusha,  ambapo vuguvugu la mgogoro huo lilianza mara baada ya kugawanywa kwa iliyokuwa halmashauri ya Arumeru na kupata halmashauri mbili za Arusha na Meru, na eneo hilo la malisho kuwa kwenye ramani ya halmashauri ya Meru.

Katika mikutano hiyo, mkuu wa wilaya ya Arumeru aliambatana na mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mhe. Ojung'u Salekwa, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, mkurugenzi mtendaji halmshauri ya Meru, Zainabu Makwinya pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Arumeru.

MATUKIO KATIKA PICHA MKUTANO WA KIJIJI CHA LOSINONI JUU NA KISIMIRI JUU WILAYA YA ARUMERU.


Mkuu wa wilaya ya Arumeru, mheshimiwa Mhandisi Richard Ruyango, akizungumza kwenye mkutano wa wananchi wa kijiji cha Kisimiri Juu kata ya Uwiro, halmashauri ya Meru, wilaya ya Arumeru.



Mkuu wa wilaya ya Arumeru, mheshimiwa Mhandisi Richard Ruyango, akizungumza kwenye mkutano wa wananchi wa kijiji cha Losinoni Juu kata ya Oldonyowasi, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.



Mkuu wa wilaya ya Arumeru, mheshimiwa Mhandisi Richard Ruyango, akitoa maelekezo kwa viongozi wa mila 'Malaigwanani' wa vijiji vya Kisimiri Juu na Losinoni Juu kwenye mkutano wa wananchi wa kijiji cha Losinoni Juu kata ya Oldonyowas halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.


Wananchi wa kijiji cha  Losinoni Juu kata ya Oldonyowas wakizungumza wakiwa kwenye mkutano wa hadhara uliongozwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru, hayupo pichani 



Mwananchi wa kijiji cha  Kiserian Juu kata ya Uwiro, akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliongozwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru, hayupo pichani 



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.