• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC ARUMERU;WAZAZI WASIOWAPATIA WATOTO WAO CHAKULA SHULENI

Posted on: February 4th, 2023

Na Rlinipa Lupembe

Wazazi halmashauri ya Arusha, wametakiwa kuhakikisha watoto wao wanapata  chakula cha mchana wawapo shuleni,  kushindwa kufanya hivyo hatua kali zitachukuliwa juu yao.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda wakati wa kikao cha tathmini ya Lishe cha robo ya pili, kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha.

Kufuatia taarifa ya tathmini ya Lishe ya robo hiyo, imeonesha asilimia 78  ya shule huku 50% tu ya wanafunzi ndio wanaopata chakula shuleni, jambo ambalo ni kiashiria hatarishi kwa afya za watoto na zaidi ni kinyume na haki za binadamu.

Mkuu huyo wa wilaya amewaagiza  Maafisa Watendaji wa kata na vijiji kusimamia shule zilizo kwenye maeneo yao na kuhakikisha kila mzazi anawajibika kwa mtoto wake ili apate chakula cha mchana awapo shuleni na kuwachukulia hatua za kisheria wazazi  wanaokaidi.

"Tumieni sheria ndogo za vijiji, kuwabana wazazi hao, kwani sera ya Elimu bila malipo imebainisha wazi, moja ya jukumu la mzazi ni kumpatia mtoto mahitaji binafsi ikiwemo chakula, vijiji visivyo na shetia ndogo hakikisheni mnazo ili kuwabana wazazi hao na watoto kupata haki yao ya msingi". Amesisitiza Mkuu huyo wa wilaya.

Aidha amewataka wazazi kutambua umuhimu wa chakula kwa afya ya mtoto, kuwa ndicho kinachojenga akili, mwili na saikolojia ya mtoto, na kuwasisitiza wazazi kuchukulia umuhimu mkubwa jambo hilo.

Akiwasilisha Taarifa hiyo ya tathmini ya Lishe kwa robo ya pili ya mwaka 2022/2023, Afisa Lishe halmashauri ya Arusha, Doto Milembe amesema kuwa mpaka sasa halmashauri inaendelea kufanya vizuri kwenye viashiria 6 kati ya 8 vilivyosainiwa na Maafisa Watendaji wa kata.

Amevitaja viashiria viwili visivyofanya vizuri ni pamoja na idadi ya watoto wanaopata chakula shuleni kuwa ni asilimia 50 tu, jambo ambalo linasababisha kiashiria hicho kupata asilimia ndogo.

"Wazazi kwa kutambua umuhimu wa lishe bora kwa watoto, wanapaswa kutimiza jukumu hilo, kwa kutambua kuwa lishe bora ina nafasi kubwa ya ufaulu wa mwanafunzi katika masomo yake, hivyo tusichukulie ni jambo rahisi hivyo, balibebwe kwa umuhimu wake.". Amesisitiza Afisa Lishe huyo.

Nao Maafisa Watendaji wa kata, wamekiri licha ya juhudi kubwa za ufuatiliaji kwa wazazi kuchangia chakula cha mchana kwa watoto wao, bado kuna changamoto ya uelewa wa baadhi ya wazazi juu ya elimu bila malipo.

Hata hivyo wameahidi kuendelea kushirikiana na viongozi wa vijiji, kamati na Bodi za shule kuwabana wazazi kutoa chakula na wale wanaokaidi kuchukuliwa hatua za kisheria.

Awali Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, ameahidi kuendelea kusimamia utekelezaji wa viashiria vyote 8 vya lishe ili kufikia malengo yaliyowekwa na serikali.

"Tukiangalia tathmini ya robo hii, matokeo yanaendelea kuboreka siku hadi siku, tutaweka mikakati ya kupandisha viashiria hivyo 2 ambavyo bado vina matokeo mabaya". Ameweka wazi Mkurugenzi Msumi

Kikao hicho cha Lishe ni cha kawaida kwa mujibu wa sheria ambapo kila Afisa Mtendaji wa kata anawasilisha taarifa ya Tathmini ya Lishe kwenye kata husika huku ikionyesha utekelezaji na  tathmini ya Viashiria 8 vya lishe vilivyowekwa na serikali.

"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"

#KaziInaendelea✍





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.