• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DC MURO ATETA NA MADIWANI ARUSHA DC

Posted on: August 23rd, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Mkuu Wilaya ya Arumeru Jerry Muro, amewataka madiwani wa Halmashauri ya Arusha, kufanya uongozi wa kimkakati kwa kujikita zaidi, kuhamasiaha wananchi wao, kishiriki kwa hali na mali shughuli za kimaendeleo na kuacha kusubiri kuihoji serikali kuwaletea maendeleo katika maeneo yao.

Akizungumza na madiwani hao, katika mkutano wa Baraza la Madiwani wa kujadili taarifa za robo ya nne na ya mwisho, kwa mwaka wa fedhe 2018/19, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo, amesema maendeleo ya nchi yoyote duniani huanzia kwa wananchi wenyewe, hivyo hamna budi kuwahamasisha wananchi wenu,  katika suala zima la kujiletea maendeleo yao.

Amefafanua kuwa, uongozi wa kimkakati ni kukaa na wananchi wako, kuweka mipango thabiti ya maendeleo katika maeneo yenu, na kuwashawishi kuanza kuitekeleza kwa kuanza kwa nguvu zao wenyewe na sio kiongozi kusubiri vikao vya halmashauri, kuhoji serikali italeta lini fedha kwa ajili ya maendeleo yenu wenyewe.

"Uongozi ni namna ya kushawishi wananchi kushiriki katika kujiletea maendeleo, na sio kazi ya kusimama na kuwatetea tu kwenye vikao, na kuisubiri serikali kuwafanyia kila kitu, imefika wakati, kiongozi kutumia nafasi yako, kuwashawishi wananchi wako kishiriki kuchangia maendeleo kwenye maeneo yenu, vinginevyo mtasubiri sana" amesema Mkuu huyo wa wilaya.

Muro amewataka madiwani hao, kuiga mfano wa madiwani wa Halmashauri ya pacha ya Meru, ambapo wao hutumia nguvu kubwa katika kuhamasisha wananchi kushiriki katika, shughuli za maendeleo na kwa kushirikisha wadau mbalimbali kutekeleza miradi katika sekta zote za Elimu, Afya, Maji na hata kukarabati miundombinu barabara za ndani wenyewe.

Akititolea mfano halisi, Mkuu huyo wa Wilaya amesema, Madiwani wa halmashauri ya Meru baada ya kuona barabara zao zimeharibika, madiwani wameamua kushirikisha wananchi na wadau wa maendeleo kuanza kuzifanyia ukarabati bila kusubiri TARURA, ambapo kwasasa shughuli za ukarabati zinaendelea katika maeneo mbalimbali ndani ya halmashauri ya Meru.

"Mkisema ninyi viongozi mnasubiri TARURA kutengeneza barabara za mitaani kwenu, mnajidanganya na kuwadanganya wananchi waliowachagua, bila kubadilika na kuchukua hatua,  nasema mtasubiri mpaka mwisho wa dahari, na muda wenu wa uongozi utakwisha na hamtarudi" amesema Muro

Aidha amewataka madiwani hao, kuacha kukodisha mitambo ya halmashauri, na badala yake kujipanga kutumia mitambo hiyo, kukarabati barabara katika maeneo yao, kwa kuwahamasisha wananchi kuchangia, pamoja na kutafuta fedha kwa  wadau wengine wa maendeleo kufanya shughuli hizo.

Hata hivyo, ameupongeza uongozi wa halmashauri hiyo pamoja na watalamu wote, kwa kutekeleza shughuli mbalimbali kisekta kwa mwaka wa fedha uliomalizika, hasa kwa kujikita kwenye maslahi ya wananchi, na zaidi katika sekta ya elimu, ambapo Januari mwaka huu wameanzisha shule mbili za sekondari, na wanatarajia kusajili shule nyingine tatu za sekondari  Likamba, Losinoni Juu na Kiserian, ambazo zinatarajiwa kupokea wanafunzi ifikapo Januari 2020 na kusisitiza kujipanga vema kuhakikisha kila tarafa inakuwa na shule ya sekondari kwa kidato cha tano na sita.

Aidha amewahakikishia waheshimiwa madiwani kuwa serikali ya awamu ya tano itaendelea kutoa ushirikiano katika kutekeleza shughuli za maendeleo kwa maeneo yote bila ya kujali itikadi za vyama vyao na kuwataka kujipanga upya kwa mwaka huu mpya wa fedha 2019/19 kuleta mabadliko ya kasi katika maeneo yao.


 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.