Na Elinipa Lupembe
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wausha, Seleman Msumi amekabidhi vyumba 38 vya madarasa kwa mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango baada ya kukamilika mradi huo uliotekelezwa kwenye shule 18 za sekondari za halmashauri hiyo.
Akizungumza wakati akisoma taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi Msumi amesema kuwa Halmashauri ilipokea shilingi milioni 760 kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 38, ikiwa ni maalum kwa maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka wa masomo unaonza Januari 2023.
Mkurugenzi Msumi amesema kuwa kiasi hicho cha fedha licha ya kutumika kujenga vyumba hivyo 38 vya madarasa, kimetumika pia kununua samani za madarasa ikiwemo viti na meza 50 kwa kila darasa pamoja na ofisi 7 za walimu kwenye shule 6 kati ya shule hizo 18.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo amebainisha kuwa jumla ya 7,857 sawa na asilimia 100 ya wanafunzi waliofaulu mtihani wa kuhitimu darasa la saba mwaka 2022, wamechaguliwa na kupangiwa kwenye shule za sekondari za serikali mwaka 2023 katika halmashauri hiyo.
"Halmashauri ya Arusha tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia kwa madarasa hayo ambayo yanakwenda kutatua changamoto ya msongamano wa wanafunzi darasani lakini pia imewaondolea kero wanachi kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa kama ilivyokuwa kawaida huko nyuma". Amesema Msumi
Aidha Mkurugenzi Msumi amefafanua kuwa mwaka 2021 halmashauri ilipokea kiasi cha shilingi Bilioni 2 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 100 vya madarasa , ikiwa madarasa 96 kwa shule za sekondari na madara 4 kwa shule mbili za msingi shikizi, madara ambayo yaliwezesha wanafunzi kujifunza katika mazingira bora zaidi na kupandisha kiwango cha taaluma kwenye shule nyingi.
Awali Mkurugenzi Msumi ameahidi kushirikiana na wazazi na walezi kuhakikisha wanzafunzi wote waliopangiwa kuendelea na masomo ya sekondari wanaripoti shuleni ifikapo tarehe 09.01.2023.
Ifahamike kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa ni utelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi Ibara ya 79 kifungu (q) Kukarabati miundombinu ya kufundishia na kujifunzia katika shule za Msingi na Sekondari nchini.
ARUSHA DC
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.