Na Elinipa Lupembe
Diwani wa kata ya Moivo, Mhe. Selina James Mollel (CCM), amekuwa Makamu Mwenyekiti halmashauri ya Arusha mara baada ya kuchaguliwa kwa kura za ndio wakati wa mkutano maalumu wa mwaka wa fedha 2021/2022.
Mwenyekiti halmashauri ya Arusha, alimtangaza mheshimiwa Selina Mollel kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha mara baada ya ya kushinda kwa kura ya ndio, na kuweka wazi kuwa kisheria Makamu mwenyekiti anashika nafasi hiyo kwa kipindi chanmwaka mmoja.
"Kwa kuwa hakuna jina la mgombea mwingine lililowasilishwa tutmelazimika kupiga kura ya ndiyo na kwa kuwa hakuna mjumbe aliyesema hapana, ninamtangaza Mheshimiwa Selina Mollel kuwa Makamu Mwenyekiti wa halmashauri na atatumikia nafasi hii kwa mujibu wa sheria,,kanuni na taratibu".Amesisitiza Mwenyekiti huyo
Mhe.Selina ameshinda kwa kura za ndio, kutokana na kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo, na kuchukua nafasi ya Mhe. Fredi Lukumay aliyehudumu nafasi ya Makamu mwenyekiti kwa kipindi cha mwaka mmoja na nusu tangu baraza hili lianze kazi mwaka 2020.
Mheshimkwa Selina, amewashukuru madiwani wenzake kwa kumuamini na kumchagua kushika nafasi hiyo na kuahidi kushirikiana na Mwenyekiti na uongozi mzima wa halmashauri kwa kuhakikisha mipango na shughuli mbalimbali za maendeleo zinasimamiwa vizuri kwa maslahi mapana ya wananchi.
Aidha Makamu Mwenyekiti huyo, amempongeza Makamu Mwenyekiti aliyetangulia kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya na kuwataka waheshimiwa madiwani kumpa shirikiano wakati wote wa kipindi cha uongozi wake ili kutekeleza majuku yake kwa wepesi ya kuwahudumia wananchi.
Hata hivyo Makamu Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, na Diwani wa kata ya Mateves Mhe. Freddy Lukumay, amempongeza makamu mwenyekiti aliyechaguliwa na kuwashukuru madiwani wote na watalamu kwa ushirikiano waliompa katika kipindi chote cha uongozi wake na kuahidi kutoa ushirikiano zaidi katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo.
Awali Mkuu wa Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu, halmashauri ya Arusha, Elizabeth Ngobei, amewasilisha taarifa na miongozi ya ichaguzi huo kuwa, unafanyika kwa mujibu wa Sheria za serikali za mitaa sura ya 287 marejeo ya mwaka 2002 na Kanuni za Kudumu za halmashauri, Makamu Mwenyekiti pamoja na wajumbe wa Kamati za Kudumu wanapaswa kuchaguliwa kila baada ya mwaka mmoja.
Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani wa mwaka, umefanyika kwa mujibu wa sheria na kanuni za serikali za mitaa, ukiwa na agenda za taarifa za maendeleo za mwaka wa fedha 2021/2022, uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti, uundaji wa Kamati za Kudumu za halmashauri pamoja na uchaguzi wa wenyeviti wa kamati hizo za kudumu.
ARUSHA DC TUPO TAYARI KUHESABIWA
SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022
JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022
PICHA ZA MATUKIO MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI
Makamu Mwenyekiti mpya halmashauri ya Arusha, mhe. Selina Molle, akiwashukuru wajumbe wa mkutano wa Baraza la Madiwani, mara baada yankumchagua kushika nafasi hiyo, wakati wa mkutano maalum wa mwaka wa Baraza la mMadiwani, kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.