• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

DR. DUGANGE: NIMERIDHISHWA NA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO ARUSHA DC...

Posted on: March 9th, 2023

Na Elinipa Lupembe.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dr. Festo Dugange, ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ambayo inaendana na thamani ya fedha ya Serikali iliyotumika na kuipongeza halmashauri ya Arusha kwa ubunifu uliotumika katika kutekeleza miradi hiyo.

Ameyasema hayo wakati akiwa kwenye ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule mpya ya sekondari kiutu, kituo cha Afya Mwandet, kituo cha afya Oldonyosambu pamoja na hospitali ya Wilaya Oltrumet.

Dr. Dugange amesema kuwa ujenzi wa shule mpya ya sekondari Kiutu unaendana na thamani ya fedha iliyotumika pamoja na ubunifu mzuri wa majengo kutokana na ufinyu wa eneo na kuongeza kuwa hali ya utekelezaji wa miradi hiyo inaridhisha licha ya kuwepo kwa mapungufu machache ya umaliziaji wa baadhi ya majengo.

“Rais Dkt. Samia Suluhu ametoa fedha nyingi kutekeleza miradi hii, hivyo Tutakuwa hatujaitendea haki fedha ya serikali kama miradi hii haitaanza kutoa huduma kwa wakati hivyo, niwatake sasa mkamilishe mapungufu madogomadogo yaliyobaki ili miradi hii ianze mara moja kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa.” Amesisitiza Dr. Dugange.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Mhe. Noah Saputu amesema kuwa serikali imesaini mikataba tayari kwa ajili ya kutengeza barabara ya kuingia kituo cha afya Mwandet pamoja na mradi wa maji utakaofika hadi maeneo ya kituo hicho cha afya ili huduma za afya ziweze kupatikana kwa urahisi Zaidi bila changamoto yoyote.

“Tunamshukuru sana Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ya kipekee anavyotujali sisi wananchi wa Arumeru Magharibi ndio maana analeta fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo kama hii ndani ya jimbo letu.” Amesema Mhe. Saputu.

Aidha, mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Arumeru, Mhe. Noel Severe ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha pamoja na viongozi wengine kwa kusimamia vyema utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi huku akiwataka wataalam wa serikali kuzunguka katika kata zote na vijiji kutekeleza majukumu yao badala ya kukaa ofisini tu.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Emmanuela Kaganda ametumia fursa hiyo kumuomba Mhe. Naibu Waziri kufikisha salamu za wana Arumeru kwa Mhe. Rais Dkt. Samia kwa kuwapatia fedha hizo za kutekeleza miradi mikubwa ya Afya na elimu ambayo itaokoa Maisha ya wananchi wengi hasa akina mama na watoto.


“Serikali imefanya sehemu yake, ni jukumu letu sasa wananchi kuitunza na kuilinda miundombinu hii ili iweze kunufaisha vizazi vya sasa na baadaye ikiwa ni pamoja na kushiriki katika kuiboresha pale itakapohitajika.” Ameongeza Mhe. Kaganda.


Awali, wananchi wa maeneo hayo wamemshukuru sana Mhe. Rais Samia kwa miradi hiyo mikubwa ambayo itaondoa changamoto iliyokuwepo ya elimu na huduma za afya na kumuomba Mhe. Naibu Waziri kuwasadia kutatua changamoto ya maji na barabara ambazo zinawakumba wananchi wa Kata za Mwandet na Oldonyosambu.


"ARUSHA DC ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga"


#kaziinaendelea✍✍✍✍

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA NAFASI ZA UDEREVA TAREHE 28/12/2018 December 19, 2018
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI DUNIANI TAREHE 1-7, AGOSTI 2020. July 31, 2020
  • TANGAZO KWA WANANCHI WOTE MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA PILI 2O20/2021 TAREHE 29.01.2021 January 29, 2021
  • KINGA TIBA YA KICHOCHO NA MINYOO YA TUMBO KWA WATOTO MIAKA 5-14 March 02, 2021
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DC ARUMERU ATEMBELEA MAENEO YALIYOPATA MADHARA YA MVUA ARUSHA DC..

    March 24, 2023
  • MVUA KUBWA YALETA MADHARA ARAFA YA MUKULAY ARUSHA DCA DC

    March 24, 2023
  • MVUA KUBWA YALETA MADHARA ARAFA YA MUKULAT ARUSHA DC

    March 24, 2023
  • DC ARUMERU AFANIKISHA MCHANGO WA MAZIWA YA MTOTO KWA KAYA ILIYOBOMOKEWA NYUMBA OLMOTONY

    March 24, 2023
  • Tazama zote

Video

MFUGAJI AKIELEZEA FAIDA ZA UHIMILISHAJI WA NG'OMBE WA MAZIWA - BANDA LA MIFUGO ARUSHA DC
Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.