Na Elinipa Lupembe
Makamu wa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ameiutaka uongozi wa Wakala wa Majengo nchini - TBA kujipanga kujietegemea katika kuendesha miradi yake na sio kutegemea ruzuku kutoka serikalini.
Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa hafla ya kuzindua jengo la makazi la kibiashara lililojengwa eneo la Sekei jijini Arusha na kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuziwezesha Taasisi zake kuwa na miradi mikubwa itakayowapa uwezo wa kujitegemea na kujiendesha yenyewe.
Aidha Dkt. Mpango amebainisha kuwa, Serikali imeiruhusu Wakala wa Majengo Nchini (TBA) kushirikiana na sekta binafsi kwa ubia ili kuipa fursa na uwanda mpana wa kutekeleza miradi ya kimkakati yenye tija na kuleta matokeo kwa haraka, itakayopunguza hali ya utegemezi kwa Serikali.
“TBA mmefanya kazi nzuri, mmejenga jengo zuri na la kisasa, kuweni na mipango endelevu ya kujenga majengo ya aina hii katika maeneo mbalimbali nchini, majengo yenye uwezo wa kuhudumia kaya nyingi zaidi kwa kuzingatia uwezo wa wananchi, uhifadhi wa mazingira, pandeni miti na maua pamoja na kuweka mifumo mizuri ya maji safi na maji taka’ amesisitiza Dkt. Mpango.
Hata hivyo ameitaka TBA kusimamia vema upangishaji wa nyumba hizo, na kuhakikisha wapangaji wanalipa kodi kwa wakati kulingana na mikaba, ili kufikia malengo ya uzazilishaji utawezesha majengo kujiendesha kibisahara na kuzalisha faida iliyokusudiwa na serikali na kuitaka Wizara ya Uwekezaji kuhakikisha inaweka msukumo kwenye ujenzi wa viwanda wa vifaa vya ujenzi, utakaopunguza gharama za ujenzi ili kuiwezesha Serikali kufikia lengo la ujenzi wa nyumba zitakazoendana na mahitaji ya ongezeko la idadi ya watu.
Naye Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema kuwa azma ya ujenzi huu ni chimbuko la TBA la kutaka kujiendesha kibiashara kwa kupata faida, hivyo imejipanga kuimisha uanzishaji wa miradi ya kimkakati yenye uwezo wa kujiendesha yenyewe na kuimarisha mfumo wa ukusanyaji kodi.
"Tumeweka mfumo wa kisaa wa vitasa janja ili kudhibiti wapangaji wadanganyifu na wenye madeni, mfumo utakaosaidia ulipaji wa kodi kwa wakati, lengo likiwa ni kupata mapato zaidi na kujiendesha yenyewe." amesisitiza Prof. Mbarawa.
Hata hivyo Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Angelina Mabula, ameipongeza TBA kwa kujenga majengo marefu yanayodhimibiti matumizi bora ya ardhi na kuhudumia idadi kubwa ya watu na kusisitiza kuwa majengo hayo yaendane na uwepo na maegesho ya magari.
Aidha amebainisha kuwa bado kuna uhitaji mkubwa wa makazi nchi, na kuweka wazi kuwa zaidi ya 390,981 zinahitajika kwa mwaka ukilinganisha na idadi ya chini ya nyumba 2000 zinazojengwa na taasisi mbalimbali kwa mwaka.
#KaziInaendeela
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.