• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

FEDHA ZA UVIKO 19 ZAONDOA MSONGAMANO WA WANAFUNZI MADARASANI SEKONDARI ILKIDING'A.

Posted on: July 18th, 2022


Na Elinipa Lupembe.

Baada ya serikali kutoa fedha za Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19, kwa ajili ya kuboresha wa miundombinu ya shule nchini, wanafunzi wamenufaika kwa kuondokana na msongamano kwenye vyumba vya madarasa.

Shule ya sekondari Ilkiding'a halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru ni miongoni mwa shule za halmashauri hiyo, iliyopokea kiasi cha shilingi milioni 220 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 11 vya madarasa pamoja na viti na meza.


Aidha kukamilika kwa ujenzi wa madarasa hayo, kumewezesha shule hiyo kuwa na vyumba vya madarasa vya kutosha kwa kuwa na uwiano wa wanafunzi 50 kwa kila darasa, uwiano ambao umeondoa kabisa msongamano wa wanafunzi darasani kama ilivyokuwa hapo awali.


Wanafunzi wa shule ya sekondari Ilkiding'a licha ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita, inayoongozwa na mama Samia Suluhu, wamethibitisha kuwa na mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishiwa, huku wakiahidi kusoma kwa bidii, kwa kuwa serikali yao makini, imewaandalia mazingira rafiki pamoja na kuwapatia elimu bila malipo.


Maurine Philemon mwanafunzi wa kidato cha nne, amekiri kuwepo kwa utulivu wa hali ya juu kwa wanafunzi wakati wa kujifunza na kufundishwa, hali iliyosababishwa na ujenzi wa vyumba 11 vya madarasa shuleni hapo kwa wakati mmoja.

"Kwa sasa tunasoma kwa nafasi na uhuru zaidi, hakuna tena msongamano, kila mwanafunzi anakaa kwenye meza na kiti chake, walimu wanatufundisha kwa kumfikia kila mwanafunzi, tunampongeza mama yetu mama Samia, zaidi tunamuombea na tunaahidi kuongeza juhudi na kufaulu masomo vizuri, kwa kweli hatutamuangusha mama" Amethibitisha Maurine


Hata hivyo wanafunzi hao wameweka wazi kuwa, miundombinu inayovutia shuleni hapo, imewezesha wanafunzi wengi kupenda shule na kupunguza utoro uliokuwepo, huku wakiahidi kuitunza miundombinu yote ya shule, ili iwasaidie wao na vizazi vijavyo.


Naye Mkuu wa shule ya sekondari Ilkiding'a, Mwl. Supeet Sailevu, amesema kuwa, mradi huo pia umesaidia walimu, kwa kufundisha idadi ya wanafunzi darasani kwa wastani unaotakiwa, zaidi  yameimarisha upimaji kitaaluma, kwa kuwa wanafunzi wote wanafanya mtihani kwa wakati mmoja sio kwa shifti kama zamani, hali iliyoondoa udanganyifu na kupandisha taaluma na kiwango cha ufaulu shuleni hapo


Ameongeza kuwa, ujenzi huo umewezesha kupatikana kwa chumba cha maktaba ya kuhifadhia vitabu na wanafunzi kujisomea, mara baada ya walimu kuachia chumba hicho kilichokuwa ofisi hapo awali.


"Kiasi hicho cha fedha, kimekamilisha ujenzi wa vyumba 11 vya madarasa, meza na viti 550, kwa kila darasa kuwa na meza na viti 50 pamoja na ofisi mbili za walimu, jambo ambalo limefanya shule hii kuwa na vyumba vya madarasa vya ziada vinavyotumika kwa shughuli nyingine za kielimu". Amesisitiza Mkuu huyo wa shule.


Awali shule ya sekondari Ilkiding'a ni moja ya shule za kata nchini zinazokuwa kwa kasi,  ilianza mwaka 1997 ikiwa na wanafunzi 80, kwa sasa ina jumla ya wanafunzi 1,627 wavulana 733 na wasichana 894.

ARUSHA DC 

KaziInaendelea

JIANDAE KUHESABIWA AUGUST 2022.

Mwalimu Tumaini Malkiori, akifundisha wanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Ilkiding'a moja ya vyumba vya madarasa vilivyojengwa kwa fedha za Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19



Wanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Ilkiding'a wakifurahia kusoma kwenye moja ya vyumba vya madarasa vilivyojengwa kwa fedha za Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19



Jengo la ghorofa mbili lililojengwa vyumba 10 vya madarasa na ofisi 2 za walimu, shule ya sekondari Ilkiding'a,  madarasa yayojengwa kwa fedha za Mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19.







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.