OR-TAMISEMI
Waziri Wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mhe.Innocent Bashungwa amewaelekeza Wakurugenzi wa Halmshauri, zinazokusanya mapato ya Ndani kuanzia shilingi bilioni 5 kwa mwaka,kuhakikisha wanatoa asilimia 10 kati ya asilimia 60, inayotengwakutekekeleza miradi ya maendeleo kwa ajili ya kuboresha miumdombinu ya Barabara lami za Mitaa.
Bashungwa, ametoa maelekezo hayo akiwa Bungeni Jijini, Dodoma wakati akijibu swali la mhe,Jerry Silaa Mbunge Ukonga, kuhusu nini kauli ya Serekali juu ya kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya kujenga barabara za lami mitaani katika mkoa wa wa Dar es Salaam.
"Nimeshatoa maelekezo kwa Halmshauri, ambazo zinatenga asilimia 60 ya mapato ya ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo kuhakikisha, wanatoa asilimia 10 kwa ajili ya kutengenezaa Barabara za Mitaa ikiwemo mkoa wa Dar es salaam"
Bashungwa,amezitaka Halmshauri hizo kushirikiana na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini Tanzania (TARURA) kuweka mpango mkakati wa pamoja kuhakikisha asilimia 10 inayotengwa, inatengeneza barabara ambazo zitaendana na uhalisia wa matumizi ya fedha.
Aidha Bashungwa amesema Serekali inaendelea,kufanya mazungumzo na Benki ya Dunia juu ya mkopo wa Miundo mbinu Katika jiji la Dar es salaam awamu ya pili (DMDP).
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.