Na. Elinipa Lupembe.
Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya Arusha Saad Mtambule, anatoa pongezi za dhati kwa Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan aliyeapishwa mapema leo, masaa machache yaliyopita, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Samia ameapishwa leo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kufariki dunia siku ya Jumatano tarehe 17.03.2021
Aidha Mheshimiwa Samia Suluhu, ameapishwa kushika madaraka ya kuiongoza Tanzania akiwa ni Rais wa sita, kufuatia Kifungu cha 37 (5) cha katiba ya Tanzania iliyotungwa mwaka 1977, kimempa madaraka kushika nafasi hiyo kwa muda uliobaki kwa kipindi cha miaka mitano.
Halmashauri ya Arusha inatoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais wa sita, Mheshimiwa Samia Suluhu Hasan na kumuombea kwa Mwnyenzi Mungu aweze kuongoza taifa letu la Tanzania kwa mujibu wa sheria kwa manufaa ya watanzania woete.
"HONGERA SANA MHESHIMIWA RAIS MAMA SAMIA SULUHU HASAAN, TUKO TAYARI KULITUMIKIA TAIFA KWA MAENDELEO YA WATANZANIA WOTE"
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.