• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

HUDUMA BORA KWA MTEJA MSINGI WA KUFIKIA MALENGO YA TAASISI HUSIKA

Posted on: October 7th, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Mkurugenzi mtendaji halmasahuri ya Arusha, Selemani Msumi, amewataka watoa huduma wote, kuendelea kuboresha hali ya utoaji huduma kwa wateja katika taasisi zao, kwa kuwa huduma kwa mteja ndio msingi wa kufikia malengo ya taasisi husika.

Amesema hayo wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa  Mteja, yaliyofanyika katika benki ya CRDB tawi la Sekei, halmasahuri ya Arusha, wilaya ya Arumeru, na kusisitia kuwa ili taasisi iweze kufikia malengo yake ya kibiashara na kijamii, lazima kipengele cha huduma bora kwa mteja kizingatiwe na kutiliwa mkaźo ili kuweza kumfanya mteja kuelendelea kuiamini taasisi inayomuhudumia.

"Tunafahamu taasisi ni nyingi na zinazotoa huduma zinazofanafa, ili kumpata mteja na kumfanya aendelee kudumu na kuiamini taasisi yako, lazima suala la huduma kwa mteja liwe imara na lenye kupewa kipaumbele, hii itasaidia taasisi kumudu ushindani mkubwa uliopo katika soko" amesisitiza Mkurugenzi huyo.

Naye Meneja wa CRDB tawi la Sekei, Winsara Ndanshau, amesema kuwa benki ya CRDB imeendelea kuwajali wateja wake kwa kutoa huduma bora huku uboreshaji wa huduma kwa mteja ukiwa ni kipaumbe, lengo likiwa kuimarisha uhusiano kati ya benki na mteja.

Winsara amezitaja huduma zinazotolewa na benki hiyo ni pamoja na huduma zote za kibenki, ikiwemo akaunti za akiba, akaunti za watoto 'Junior Jumbo', akaunti maalumu kwa wanawake 'Malkia Akaunti'  akaunti za wafanayakazi,  wafanyabishara wakubwa na wadogo, mikopo kwa wafanyakazi wa serikalini, wafanyabiashara wakubwa, mikopo kwa wafanya biashara wadogo 'wajasiriamali'  mikopo kwa wakulima sambamba na huduma za bima ya maisha, afya, majengo na vyombo vya moto.

Hata hivyo baadhi ya wateja wa CRDB walioshirikia hafla hiyo, baada ya kufika tawini hapa kupata huduma, wameipongeza benki hiyo kwa kutoa huduma bora, huduma ambazo hupatikana kwa wakati pindi mteja anapohitaji, jambo ambalo linawafanya kuendelea kuiamini benki hiyo inayowajali wateja wake.

Ian Cherles mteja wa CRDB tawi la Sekei, ameweka wazi kuwa yeye hufika kwenye tawi hilo mara kwa mara kupata huduma za kibenki na hajawahi kupata mkwamo, na kuongeza kuwa hata pindi inapotokea changamoto yoyote, hupata utatuzi wake kwa haraka na kwa wakati, kutokana na benki hiyo kuwa na huduma bora kwa wateja.

Awali,maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja hufanyika wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba kila mwaka, Kauli mbiu ya maadhimisho hayo mwaka 2021 ni *Nguvu ya Huduma*, huku benki ya CRDB tawi la Sekei ikijumuika na wateja wake, katika hafla fupi ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Mteja katika benki hiyo.


MATUKIO KATIKA PICHA


Mkurugenzi Mtendaji halamshauri ya Arusha ( wa kwanza kushoto) na Meneja wa CRDB tawi la Sekei Winsara  Ndanshau, wakikata keki, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Mteja katika tawi hilo la Sekei.

Baadhi ya wateja wa Benki ya CRDB tawi la Sekei wakipata huduma wakati wa maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Mteja katika tawi hilo la Sekei


Baadhi ya wateja wa Benki ya CRDB tawi la Sekei wakimsikiliza mgeni rasmi, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa Mteja katika tawi hilo la Sekei





Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.