• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

JAMII IMETAKIWA KUDHIBITI MAWASILIANO YA KIDIGITALI KWA WATOTO ILI KUKABILIANA NA MMOMONYOKO WA MAADILI...

Posted on: June 15th, 2023

Na Elinipa Lupembe 

Jamii imetakiwa kuwadhibiti watoto dhidi ya  matumizi ya teknolojia ya ya mawasiliano mtandao, ili kukabiliana na ulimwengu wa digitali, teknolojia ambayo imeaminika kuwa na kasi ya kumomonyoa maadili kwa jamii huku watoto wakiwa wakiathirika wakubwa.


Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya Arumeru Mhe. Emmanula Mtatifikolo Kaganda, wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika halmashauri ya Arusha, zilizofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Loovilukuny Kata ya Kisongo.


Amewataka wazazi kuzingatia usalama wa watoto dhidi ya matumizi ya simu janja, komputa na televisheni kwa kuwa, vifaa hivyo vya kiditali vina mambo mengi mazuri na mabaya, ambapo watoto huvutiwa zaidi na mambo mabaya, ambayo huathiri tabia za watoto kwa kuiga na kufanya mambo hayo katika maisha yao ya kawaida, tabia ambazo ni kinyume na maadili ya jamii za kitanzania.


Amefafanua kuwa, licha ya maadili kumomonyoka kupitia matumizi ya digitali, hatuwezi kuishi nje wala kujitenga nayo, ila wazazi na walezi mnalo jukumu kubwa la kudhibiti na kuwasimia watoto na kuhakikisha wanafanya matumizi salama ya digitali kwa kuzingatia  usalama wa mtoto ili kuwaepusha watoto na madhara yanayotokana na mambo mengi yanayopatikana mtandaoni.


"Wazazi tusione sifa watoto kuiga tabia za kimagharibi, tutunze tamadumi zetu, jukumu letu kubwa ni kuhakikisha maisha ya watoto yanakuwa salama kwa kuwa digitali ndio mfumo wa maisha ya sasa, hutuwezi kujitenga nao, la msingi ni wazazi na wadau kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha  watoto wetu wawe salama kupitia uwepo wa digitali katika maisha yetu" Amesisitiza Mhe. Emmanuela.


Awali wakisoma risala, watoto wamelalamikia matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kusababisha vitendo vya ukatili vinavyofanyika dhidi ya watoto huku watoto wakifanya ngono katika umri mdogo huku wengine  wakilawitiana wenyewe kwa wenyewe na kuwaomba wazazi, walezi na mamlaka za serikali kusimamia maadili ya mitandaoni.


"Watoto tunasikitishwa sana vitendo vibaya vinavyofanywa na watoto, kutokana na matumizi ya mitandao ya mawasiliano, kumekuwa na wimbi la watoto kujiingiza kwenye ngono, katika umri mdogo huku wengine wakilawitiana wenyewe kwa wenye, tunaomba serikali kusimamia maudhui ya watoto mitandaoni" Ameweka wazi msoma Zenufa Said


Hata hivyo wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mtoto (MTAKUWWA) kijiji cha Loovilukuny wamethibitisha tabia ya wazazi kwa kisasa kutumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii na kutelekeza majukumu yao ya kusimamia watoto, jambo ambalo linaathiri sana tabia za watoto.


"Baba na mama wako bize kwenye simu zao, wakiwaacha watoto wakiangalia katuni na michezo mingi kwenye mtandao, tabia ambazo zimeongeza kasi ya mmomonyoko wa maadili kwa watoto ni vyema wazazi kurejea kwenye mstari wa malezi.


Halmashauri ya Arusha kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya mtoto, imeadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika 2023 yenye Kauli Mbiu ya  "Zingatia Usalama wa Mtoto katika Ulimwengu wa Kidigitali"


ARUSHA DC Ni Yetu, Tushirikiane Kuijenga



Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.