• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Jamii ya wafugaji imetakiwa kupaza sauti na kukemea vitendo vya ukatili dhidi ya watoto

Posted on: April 8th, 2019

Na Elinipa Lupembe.

Viongozi wa jamii ya wafugaji yenye asili ya kabila la kimaasai, wametakiwa kuongeza kasi ya kupaza sauti, kwa kuendelea kuelimisha,  kuhamasisha jamii zao, kuachana na mila potofu, zinazomkandamiza na kuwakosesha mtoto wa haki za msingi.

Wito huo umetolewa, wakati wa semina ya siku moja ya kuutambulisha mradi mpya wa SAUTI YANGU, iliyowakutanisha wadau mbalimbali kwenye ngazi ya kata wakiwemo, viongozi wawakilishi wa wananchi na viongozi wa serikali, viongozi wa mila na viongozi wa dini, wa kata za Kimnyaki na Mwandet, semina iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Arusha.

Akizungumza wakati wa semina hiyo, mkurugenzi wa shirika la  Centre for Women and Youth Development (CWCD) Tanzania, Hindu Mbwego, amewataka viongozi hao wa jamii ya wafugaji, kupaza sauti zao kwa kuendelea kuelimisha jamii yao, kubadilika na kuachana na mila potofu, zinazowakandamiza watoto kwa namna moja au nyingine na kuwa na uwajibikaji rafiki kwa watoto utakaowawezesha watoto kuwa huru na wazi mbele ya jamii.

Amewasisitiza kukemea vitendo vinavyofanywa na jamii hiyo kwa kivuli cha mila na desturi na kuvitaja vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto, ni pamoja na watoto wa kike kuchumbiwa wakiwa shuleni, ndoa za utotoni, kukeketa pamoja na ufanyishwaji wa kazi ngumu kwa watoto na kuhakikisha watoto wanapatiwa mahitaji yao ya msingi.

Hindu amefafanua kuwa, mradi wa SAUTI YANGU, unalenga kuhakikisha jamii ina uelewa wa pamoja juu ya haki za mtoto, huku ukiwataka watoto wenyewe kutambua haki zao na kuzisimamia, wakiwa na uwezo wa kutoa taarifa juu ya matukio ya kikatili dhidi yao.

Hata hivyo wadau hao, wamekiri kuwepo kwa vitendo  hivyo vya ukatili dhidi ya watoto na kuthibitisha kuwa vitendo hivyo, hufanywa na jamii yao kutokana na mila na desturi za kabila lao, ambazo kimsingi wamezaliwa na kukuta wazee wao wakizitekeleza na kuongeza kuwa kutokana na elimu wanayoipata, wanaendelea kuelimishana na kuachana na mila hizo.

Diwani wa Kata ya Mwandet, mheshimiwa Boniface Tarakwa, amethibitisha uwepo wa ukatili dhidi ya watoto kwenye kata yake, unaotokana na mila na desturi za kabila lao, ikiwemo ndoa za utotoni na kuongeza kuwa, viongozi wanafanyakazi kubwa kuelimisha jamii yao, na tayari watu wameanza kubadilika, huku akiamini siku zinavyokwenda mila hizo zitakwisha.

"Ni kweli matukio ya ukatili dhidi ya watoto, hasa ndoa za utotoni yapo kwenye jamii yetu, na hii inatokana na mila ambazo tulikuta wazee wetu wanachumbia msichana kuanzia mimba, lakini kwa sasa jamii imeanza kutambua ni udhalilishaji na ni kosa kisheri, wengi wameanza kubadilika" amesema Diwani huyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri, mheshimiwa, Noah Lembris, amesema kuwa ukatili dhidi ya watoto, hawezi kwisha kama jamii yenyewe haitakubali kubadilika kimtazamo, kuanzia mtu mmoja mmoja kwenye ngazi ya familia, kwa kuwa haki za watoto wengi zinapotezwa na watu wa ndani ya familia.

"Kesi nyingi za ukatili dhidi ya watoto, zinashindwa kuwapa haki watoto, kutokana na wazazi kukubaliana kumalizana nyumbani na kuacha kuhudhuria mahakamani kutoa ushahidi kwenye kesi hizo.

Wakili wa Serikali, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mkoa wa Arusha, Mweneti Azael, amesisitiza jamii hiyo kutambua kuwa, haki na Wajibu wao kama wazazi kwa mtoto vinakwenda sambamba, na utekelezaji wake ukienda sawa,  ukatili wa mtoto utakuwa umetokomezwa.

Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Arusha, Getrude Darema, amesema kuwa, mafunzo hayo, yametolewa na halmashauri kwa kushirikiana na shirika la CWCD, kwa lengo la kuwajengea uwezo na maarifa ya ufahamu juu ya haki na ulinzi wa mtoto, ukatili dhidi ya mtoto, kuchambua utendaji wa mfumo wa ulinzi wa mtoto pamoja na kuchukua hatua kwenye vikwazo vya masuala mazima yanayomhusu mtoto.

Awali, Mradi huo wa SAUTI YANGU,  unatekelezwa na shirika la CWCD kwa ufadhili wa shirika la Child Fund la nchini Korea, kwenye kata mbili za Mwandet na Kimnyaki.




Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.