• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

JAMII YATAKIWA KUFAHAMU UMUHIMU WA LISHE BORA KWA MAMA ANAYENYONYESHA

Posted on: August 9th, 2022

Na Elinipa Lupembe


Halmashauri ya Arusha imeungana na mataifa yote duniani, kuadhimisha wiki ya Unyonyeshaji Dunia, kwa kutoa elimu kwa kina mama na jamii, umuhimu wa unyonyeshaji na lishe bora kwa mama anayenyonyesha kwa kipindi cha miaka miwili.

Elimu hiyo imetolewa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na mikutano ya jamii, huku  jamii ikielimishwa kufahamu umuhimu wa lishe bora kwa  mama anayenyonyesha, kutokana na uhitaji mkubwa wa virutubisho mwilini, kwa ajili ya afya yake na kutengeneza maziwa ya mtoto anayemnyonyesha kwa kipindi chote cha kunyonyesha.

Mratibu wa Mama na Mtoto, halmashauri ya Arusha, Butolwa Bujiku, amefafanua kuwa ni muhimu mama anayenyonyesha kula milo kamili zaidi ya mitatu kwa siku na akiongeza asusa katikati ya milo hiyo mitatu.

Bujiku ameongeza kuwa ulaji unaofaa kwa mama anayenyonyesha, humfanya mama kuwa na afya bora na humpatia virutubisho vya kutosha kutokana na ongezeko la mahitaji ya virutubishi wakati wa unyonyeshaji, ambavyo huwezesha mwili wake kutengeneza na kutoa maziwa ya kutosha kadri mtoto anavyohitaji kwa kipindi chote cha miaka miwili.

Aidha lishe bora huimarisha kingamwili ya mama dhidi ya maradhi mbalimbali, kuzuia upungufu wa damu zaidi huongeza akiba ya madini chuma ambayo hutumika kwa mama na kwa mtoto kupitia maziwa ya mama.

"Mama akipata lishe bora kwa kipindi chote cha unyonyeshaji, atakuwa na maziwa yakutosha,  yanayomuwezesha mtoto kuwa na afya bora na kukua vizuri kimwili, kiakili na  kisaikolijia na zaidi maziwa ya mama huimarisha kinga  ya mama na mtoto dhidi ya magonjwa na kujenga akili ya mtoto.

Naye Afisa Lishe halmashauri ya Arusha Doto Milembe, ametaja mlo kamili unatakiwa angalau kuwa na mchanganyiko chakula kimoja kutoka makundi matano ya vyakula ikiwemo wanga na mizizi, nyama, mafuta, mbogamboga, matunda, virutubisho vyenye madini ya chuma, maji  na chumvi yenye madini joto.

Ameongeza kuwa ulaji wa vyakula vyenye asili ya wanyama kama nyama, kuku, mayai, maziwa, samaki, dagaa vina virutubisho kwa wingi ikiwemo protini na madini chuma ambayo husaidia kuongeza damu mwilini, na kusisitiza ulaji wa matunda ya aina mbali mbali na mbogamboga kwa wingi una vitamini kwa wingi ambazo huongeza kinga mwilini.

Afisa Lishe huyo amesisistiza mama anayenyonyesha kunywa maji ya kutosha angalau Lita moja na nusu kwa siku, pamoja na kumeza vidonge vya kuongeza damu (FEFO) kwa kipindi cha miezi 3 baada ya kujifungua.

Hata hivyo Kaimu Mganga Mkuu, Halmashauri ya Arusha Dkt. Japhet Champanda, amebainisha kuwa mama anayenyonyesha licha ya kupata lishe bora anatakiwa kujikinga dhidi ya magonjwa ya kuambukiza kama vile malaria kwa kulala kwenye chandarua kilichowekwa dawa na kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya zinaa na virusi vya UKIMWI.

Dkt. Champanda amesisitiza kuwa,  ni muhimu mama anayenyonyesha kusaidiwa kazi nzito ili apate muda wa kutosha wa kupumzika na kumnyonyesha mtoto mara kwa mara kila anapohitaji, usiku na mchana.

Awali kilele cha maadhimisho ya Wiki ya unyonyeshaji kitaifa yatafanyika mkoani Singida yakiwa na  Kauli Mbiu ya "Chukua  hatua endeleza unyonyeshaji: Elimisha na toa Msaada".


SHIRIKI SENSA YAWATU NA MAKAZI 2022.

JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022



Muuguzi kituo cha Afya Oldonyosambu akimuelekeza mama namna ya kumnyonyesha mtoto, ikiwa ni shughuli za Maadhimisho ya wiki ya Unyonyeshajio Duniani katika Halamshauri ya Arusha.




Muuguzi Kituo cha Afya Oldonyosambu Vaileth Chahe, akitoa Mafunzo ya umuhimu wa unyonyeshaji na lishe bora kwa mama na mtoto, ikiwa ni shughuli za Maadhimisho ya wiki ya Unyonyeshajio Duniani, halmasahuri ya Arusha.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.