• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji yatembelea na kukagua miradi ya maji Arusha DC

Posted on: March 20th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Kamati ya kudumu Bunge  ya kilimo, mifugo na maji imeipongeza Halmashauri ya Arusha, kwa juhudi kubwa zilizofanyika katika utekelezaji wa mirafi ya maji ya vijiji kumi iliyokuwa ikifadhiliwa na Benki ya Dunia, wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo katika halmashauri hiyo.

Kamati hiyo imetembelea mradi wa maji wa Loovilukuny uliokamilika kwa asilimia 95%  na mradi wa maji wa Ngaramtoni uliokamilika kwa asilimia 100% iliyogharimu kiasi cha shilingi Bilion 1.4 mpaka sasa.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo Mheshimiwa,  Mahammud Mgimwa, amesema kuwa,  halmashauri ya Arusha ni moja ya halmashauri iliyofanya vizuri katika utekelezaji wa miradi ya maji ya vijiji kumi, juhudi zilizowezesha, mafanikio makubwa katika miradi ya maji.

Mwenyekiti huyo, amezitaka halmashauri nyingine hapa nchini, zinazotekeleza miradi hiyo ya maji kuiga mfano wa halmashauri ya Arusha, kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa kufuata taratibu zilizopo.

"Halmashauri ya Arusha ni miongoni mwa halmashauri chache zilizotekeleza miradi ya maji ya vijiji kumi, kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na Halmashauri zingine hapa nchini, halmashauri nyingine hazibudi kuiga utendaji kazi wa halmashauri hii" amesema Mh Mgimwa.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Muro amesema kuwa, kwasasa wananchi wa halmashauri ya Arusha wanapata maji safi, kwa asilimia 57.9% na wanatarajia kufikia asilimia 61.67% pindi miradi yote iliyosalia itakapokamilika.

Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Dk. Wilson Mahera amebainisha siri kubwa ya mafanikio, katika utekelezaji wa miradi hiyo, ni pamoja na usimamizi makini wa siku hadi siku, usimamizi wa matumizi sahihi ya pesa,  kuwashirikisha wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

"Tumekuwa na usimamizi wa karibu wa utekelezaji wa miradi na matumizi ya fedha pamoja na kuwatumia wadau mbalimbali, wataalamu pamoja na wananchi kwa kuwaweka pamoja katika kutekeleza miradi hii na ndio sababu tumefikia hapa" amesema Dk. Mahera

Nao wananchi wa Ngaramtoni, hawakuwa nyuma kuishukuru serikali ya awamu ya tano, inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa usimamizi thabiti wa miradi ya maendeleo inayowanufaisha zaidi wananchi wa hali ya chini ambao ndio wahitaji zaidi.

John Mollel mkazi wa Ngaramtoni amesema kuwa, tunaishukuru sana serikali ya awamu ya tano, serikali ambayo imejikita kwenye kuwahudumia wananchi  wa hali ya chini na kuongeza kuwa miradi hiyo ya maji imewanufaisha wanchi ambao walikuwa wakiteseka na upatikanaji wa majibyasiyo ya uhakika kwa kipindi kirefu.

Awali jumla ya miradi minne kati ya kumi imekamilika, ikiwemo mradi wa maji Ilkirevi, na Oloigueruno, Nduruma, Loovilukuny na Ngaramtoni, na tayari wananchi wameanza kupata maji, huku miradi mingine sita iko kwenye hatua mbalimbali za utekelezaji na inategemea kukamilika kabla ya mwaka ujao wa 2020.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.