• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

ARUSHA DC YATOA TUZO KWA WALIMU NA WADAU WA ELIMU; KILELE CHA MAADHIMISHO YA JUMA LA ELIMU 2023

Posted on: June 2nd, 2023

Na Elinipa Lupembe

Halmahauri ya Arusha imeadhimisha Juma la Elimu 2023 kwa kutoa tuzo kwa walimu na wadau wa elimu wanaochangia  kukuza taaluma na kuongeza kiwango cha ufaulu kwa shule za msingi na sekondari.

Jumla ya walimu 40 wamekabidhiwa vyeti na nishani kwa weledi wao katika kufundisha na kuwezesha ufaulu mkubwa wa wanafunzi kwa masomo wanayofundisha huku
wadau wa elimu, kutoka mashirika 14 wakipewa zawadi za uchangiaji sekta ya elimu katika halmashauri hiyo.

Akikabidhi zawadi hizo, Mgeni rasmi na Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhe. Emmanuela Mtatifikolo Kaganda, licha ya kuwapongeza wanafunzi, walimu, wazazi na wadau wote wa elimu kwa kuwezesha halmashauri hiyo kufanya vizuri kitaaluma hususani kwenye mitihani ya wilaya, mkoa na Taifa, amewataka kuendelea kujitoa kwa hali na mali kuhakikisha watoto wa kitanzania wanapata elimu bora kwenye mazingira wezeshi.

"Serikali inatambua na kuthamini kazi kuwa inayofanywa na walimu ya kuondoa ujinga kwa wanafunzi licha ya changamoto nyingi zinazowakabili walimu, lakini juhudi zenu katika kukuza taaluma, zinathibitisha uzalendo mlio nao kwa nchi yenu, endeleeni kusimamia nidhamu na madili pamoja na usalama wa watoto wetu wawapo shuleni, niyashukuru mashirika yote na niwatake tuendelee kufanyakazi kwa weledi na kufikia malengo ya serikali" Amefafanua mkuu huyo wa wilaya.

Hata hiyo kaimu Afisa Elimu Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha, ameweka wazi kuwa, wilaya Arumeru kupitia halmashauri zake mbili za Arusha na Meru, ndio zinaubeba mkoa huo kwa kufanya vizuri kwenye sekta ya elimu ikiwemo kitaaluma, utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo, utunzaji wa mazingira pamoja michezo kwa shule za msingi na sekondari.

"Ukiangalia shule zinazofanya vizuri kwenye mitihani ya mkoa na Taifa ziko Arumeru,  mkoa unajivunia usimamizi imara wa fedha za serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo lakini zaidi kwenye suala zima la michezo ambapo mkoa unabebwa na wilaya hii ya Arumeru" Amebainisha Afisa huyo

Hata hivyo walimu na wadau wa elimu, wameishukuru na kuipongeza ofisi ya mkuu wa wilaya kupitia halmashauri ya Arusha   kwa tuzo hizo zinazothibitisha kuthaminiwa kwa kazi kubwa inayofanywa na wadau wa elimu hudusani walimu wanaopambana na wanafunzi na kuhakikisha taifa linakuwa na wasomi wenye kutumia mbinu, stadi na maarifa katika kutumikia taifa kwenye sekta mbalimbali.

Mwalimu wa kujitolea shule ya sekondari Oldonyosambu, Mwl. Mathayo Meigaru, aliyepata zawadi ya kufanya vizuri katika kufundisha somo la Hisabati, amesema kuwa zawadi hizo ni motisha kubwa kwa walimu, inayowapa ari kuwaongezea juhudi na maarifa katika kazi, na kuahidi kuendeleza kuipigania nchi yake kupitia taaluma yake ya ualimu.

Naye Mratibu wa miradi, shirika la ACE Africa, Lukuba Mbozi, licha ya kuishukuru serikali kwa kutambua na kuthamini mchango wa wadau, amethibitisha kuwa zawadi hizo ni chachu ya maendeleo ya kusukuma zaidi gurudumu hilo, ili kufika malengo ya serikali ya kuhakikisha kila mtoto wa kitanzania anapata elimu bila kujali hali zao za kimaisha.

Halmashauri ya Arusha, imeathimidha Juma la Elimu 2023, kwa kutoa tuzo kwa walimu na wadau wa elimu katika halmashauri hiyo.

*ARUSHA DC Ni Yetu,Tushirikiane Kuijenga"
#KaziIendelee




















 


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.