• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

KLABU YA ROTARY YA NCHINI DENMARK YAKABIDHI MAABARA NA MADARASA SEKONDARI OLDONYOWASI.

Posted on: September 17th, 2021

Na.Elinipa Lupembe.

Klabu ya Rotary inayoundwa na wananchi wa kijiji cha Landsbay cha nchini Denmark kwa kushirikiana na Klabu ya Rotary ya Njiro jijini Arusha, imeendelea kuboresha miundo mbinu ya shule ya sekondari Oldonyowas, halmashauri ya Arusha wilayani Arumeru, tangu kuanzishwa kwa ujenzi wa shule hiyo mpya mwaka 2017, baada ya kukabidhi vyumba viwili vya madarsa na maabara ya somo la Kemia na Baiolojia  kwa serikali.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano na uzinduzi wa majengo hayo mawili,kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Arumeru, Eng. Richard Ruyango, mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha Selemani Msumi, amewashukuru wananchi wa Denmark wanaounda klabu hiyo, kwa kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita, kuboresha miundombinu ya elimu, na kuhakikisha watoto wa kitanzania wanasoma katika mazingira bora na salama.

Hata hivyo mkurugenzi Msumi, licha ya kupongeza juhudi za Klabu hiy, amewataka walimu na wanafunzi kutambua thamani ya majengo hayo, kwa kuyatunza na kuongeza bidii katika kupandisha kiwango cha taaluma shuleni hapo, huku akiwasisitiza wanafunziwa shule hiyo, kusoma kwa bidii, kwa kuwa tayari serikali imesimami uwepo wa mazingira rafiki ya kufundishia na kujifunzia.

"Jukumu lenu wanafunzi kwa sasa ni kuhakikisha mnasoma kwa bidii, na kufaulu vizuri katika masomo yenu, kwa kuwa tayari mazingira ya kujifunzia ni rafiki, wekeni nidhamu mbele 'be ethical, do right thing' fuata maadili tenda kwa usahihi, lakini pia onyesheni juhudi ili kuwatia moyo, wananchi wa Denmark waweze kuendela kuwasaidia, wananchi wa Denmark wamejitoa kwa moyo, msiwakatishe tamaa" amesisitiza Mkurugenzi Msumi

Naye mwakilishi wananchi wa kijiji cha Lasbay nchini  Denmark, Jespa Gregersen, amesema kuwa Klabu hiyo imefanikisha kukamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na samani zake kwa gharama ya shilingi milioni 54, huku jengo la maabara na miundombinu yake likighatimu kiasi cha shilingi milioni 64, majengo ambayo yamekamilika na yamezinduliwa na kukabidhiwa kwa serikali, tayari kwa kutumiwa na wanafunzi wa Oldonyowas.

Amefafanua kuwa lengo la ujenzi wa miundombinu hiyo shuleni hapo, ni kuwawezesha wanafunzi kupata elimu katika mazingira bora, na kuahidi kuwa hivi karibuni klabu hiyo inakusudia kuanza ujenzi wa bwalo la chakula na jiko, lengo likiwa kuwawezesha wanafunzi kupata chakula kwenye mazingira rafiki pia, kwa kuwa elimu bora inaenda sambamba na afya bora.

"Ninawashukuru wananchi wa kijiji cha Oldonyowas kwa kunipa ushirikiano mkubwa, katika kila hatua ya maendeleo tunayopanga pamoja, tunakufikia malengo kwa wakati, ninaamini  ujenzi wa majengo hayo yote, umewezekana kutokana na wananchi wa kijiji hiki, kuwa na kiu sana ya maendeleo" amesisitiza Jespa mdau huyo wa maendeleo.

Hata hivyo mwenyekiti wa kijiji cha Oldonyowas Mheshimiwa Geophray Ayo, licha kuishukuru klabu hiyo ya Rotary kupitia Bwana Jespa, amemuomba kutokuchoka kuendelea kuisaidi shule hiyo mpya, kwa kuwa bado inakabiliwa na upungufu wa baadhi ya miundombinu muhimu ikiwemo Maktaba pamoja na bweni la wanafunzi kiume, watoto ambao hutembea umbali mrefu kwenda na kurudi shule kila siku, jambo ambalo linakatisha tamaa kwa baadhi ya wanafunzi kuendelea na shule.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi wa shule ya sekondari Oldonyowas, Rais wa serikali ya wanafunzi Mika Ismail (kidato cha III), ameishukuru klabu hiyo ya Rotary kwa misaada wanayoitoa kwa shule yao, na kuahidi kuyatunza majengo hayo, pamoja na kuhimiza wanafunzi wote kuongeza bidii katika masomo yao ili  kupandisha kiwango cha taaluma na ufaulu wa shule hiyo katika matokeo ya mitihani ya ndani na ile ya kitaifa.

Klabu hiyo ya Rotary ya nchini Denmark imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo katika kijiji cha Oldonyowas tangu mwaka 1992 na imefanikiwa kuwekeza miradi katika seka ya elimu, afya na maji, kwa kujenga mradi wa maji, zahanati pamoja na kushiriki bega kwa bega katika mipango ya uanzishwaji wa ujenzi wa shule hiyo ya sekondari ya Oldonyowas.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, anaendelea kuwakaribisha wadau wa maendeleo ndani na nje ya nchi, kusaidia kuboresha miundombinu ya shule za sekondari na msingi katika halmasahauri ya Arusha.


HABARI KATIKA PICHA 

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi (kushoto) na Mwakilishi wa Rotary Klabu ya Denmark, Jespa Gregersen, wakizindua jengo la vyumba viwili vya madarasa, shule ya sekondari Oldonyowas, wakati wa hafla ya kukabidhi majengo hayo kwa serikali.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akiwa ndani ya darasa jipya, shule ya sekondari Oldonyowasi, mara baada ya kuzinduliwa na kukabidhiwa jengo hilo na mwakilishi wa Klabu ya Rotary inayoundwa na wananchi wa kijiji cha Landsbay cha nchini Denmark bwana Jespa Gregersen (hayupo pichani).

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Selemani Msumi (kushoto) na Mwakilishi wa Rotary Klabu ya Denmark, Jespa Gregersen, wakizindua jengo la Maabara ya Kemia & Baiolojia, shule ya sekondari Oldonyowas, wakati wa hafla ya kukabidhi majengo hayo kwa serikali


Wanafunzi wa kidato cha tatu, shule ya sekondari Oldonyowas, Linda Mgimba (wa kwanza kulia) na Venancia Metishili wakielezea matumizi ya vifaa vya maabara na namna ya kuchanganya kemikali mbalimbali kwa kutumia vifaa hivyo vya maabara, mara baada ya jengo la maabara hiyo kuzinduliwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.