• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maabara zaanza kuongeza ufaulu masomo ya Sayansi Sekondari Osiligi

Posted on: May 21st, 2018

Baada ya agizo la serikali la kujenga maabara za masomo ya Sayansi katika shule zote za sekondari, maabara hizo zimeanza kuzaa matunda kwa kuwa na ongezeko la wanafunzi katika maso ya Sayansi pamoja na ongezeko la ufaulu pia.

Shule ya sekondari Osiligi kata ya Olturumet moja ya shule iliyopata maabara baada ya agizo la serikali, maabara hiyo imewezesha ongezeko la ufaulu kwa wanafunzi katika masomo hayo kulinganisha na miaka ya nyuma kabla ya uwepo wa maabara.

Hayo yamethibitishwa na mkuu wa shule  ya sekondari Osiligi, mwalimu Rosemary Tiganyira alipozungunza na mwandishi wa habari hizi alipotembelea shule hapo.

Mkuu huyo wa shule amesema kuwa, tangu kujengwa maabara ya masomo ya Sayansi mwaka 2016, wanafunzi wameanza kufanya vizuri katika masomo hayo tofauti  na hapo awali kulipokuwa hakuna maabara.

Mwalimu Tiganyira, ameongeza kuwa  licha ya kuwa na wanafunzi wachache wanaochagua masomo ya sayansi na kuwa na walimu wachache lakini bado wanafunzi wanaonesha kufanya vizuri tofauti na masomo ya Sanaa yenye walimu wengi.

Amesema kuwa kwa matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne ya mwaka 2017, wanafunzi  47 waliofanya mtihani wa Biolojia, walifaulu wote kwa alama A mpaka D, wanafunzi 14 kati ya 18, walifaulu somo la Kemia na wanafunzi 7 kati ya 18 nao walifaulu somo la Fizikia kwa alama A mpaka D.

Hata hivyo mkuu huyo wa shule amethibitisha kuwa, wanategemea wanafunzi wa kidato cha nne watakaofanya mtihani mwaka huu kupata matokeo mazuri zaidi hasa wakiangalia matokeo ya mitihani ya ndani.

" Wanafunzi kwa sasa wanafurahia masomo ya Sayansi na wanafanya vizuri, tunategemea kiwango cha ufaulu kuongezeka kwa kuwa, hata mayokeo ya mitihani ya ndani, wanafunzi wanafanya vizuri" amesema mkuu huyo wa shule

Naye Meshaki Saruni mwanafunzi wa kidato cha nne amesema kuwa, uwepo wa maabara unawasaidia kulipenda somo, kujiamini kwa kile wanachokifanya na zaidi vitendo vinawawezesha kukumbuka kile walichojifunza.

Ninapofundishwa darasani, nikaenda maabara kufanya practical na kuthibitisha kile nilichokisoma, inanifanya kulipenda sana somo, kuamini kile nilichojifunza na sio rahisi kusahau, tofauti na kujifunza bila practical" amesema Meshaki.

Mwanafunzi Meshaki amewataka wanafunzi kutokuogopa masomo ya Sayansi  kwa kuyaona ni magumu na kuwaondoa wasiwasi kuwa kama kuna maabara, masomo ya Sayansi ni marahisi mno.

Licha ya wanafunzi hao kuanza kufanya vizuri katika masomo ya Sayansi lakini bado kuna changamoto ya upungufu wa walimu wa masomo ya Sayansi.

Halmashauri ya Arusha inaendelea kukamilisha ujenzi wa maabara kwenye shule 27 za serikali huku ikiwa na jumla ya vyumba 74 vya maabara za masomo ya Fizikia, Kemia na Biolojia huku ikiwa na upungufu wa vyumba 7 vya maabara.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.