Na Elinipa Lupembe
Wakurugenzi halmashauri ya Arusha Seleman Msumi na Halmashauri ya Meru Mwl. Zainabu Makwinya, zote za Wilaya ya Arumeru wakianagalia kuku aina ya silki wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini Eneo la Themi Njiro Jijini Arusha.
Mabanda ya Halmashauri za Arusha na Meru yamesheheni watalamu, wakulima na wafugaji kwa ushirikiano wakitoa elimu ya teknolojia mbalimbali za kilimo ikiwemo matumizi ya teknolojia za kisasa za kilimo, matumizi ya mbegu bora, utunzaji wa mashamba na mazao shambani, udhibiti wa magonjwa ya mazao, utunzaji wa mazao pamoja na mnyororo wa thamani kufikia Ajenda 10- 30 Kilimo Biashara.
Aidha katika mabanda ya Mifugo kumesheheni teknolojia za wanyama hai, vifaa vya kusindika mazao ya wanyama maziwa, mayai, nyama na ngozi, mnyororo wa thamani kupitia mazao ya mifugo, Nishati ya kinyesi cha wanyama 'iogas' , teknolojia ya Uhimilishaji ng'ombe uzalishaji wa kupandikiza kupitia chupa , usajili wa mifugo kwa njia ya kielekroniki kwa pamoja ni kufikia Ajenda ya 10 -30 Kilimo ni Biashara.
Wakurugenzi hao wamebainisha kuwa, Serikali kupitia halmasahuri zao za Arusha na Meru zinawawezesha wakulima na Wafugaji kutumia teknolojia za kisasa katika kilimo ili kufikia Ajenda 10-30 ya Kilimo Biashara.
Ili kufikia Ajenga10-30, Wakurugenzi hao kwa pamoja wamewataka wafugaji na wakulima wa halmashauri hizo, kuwatumia Maafisa Ugani katika maeneo yao, ili kupata utalamu na mbinu na teknolojia za kisasa kufanya kilimo cha kisasa chenye tija kwa maendeleo yawakulima na Taifa kwa ujumla.
Aidha wakurugenzi hao wanawakaribisha wafugaji na wakulima wote kutembelea mabanda yao kwenye maonyesho na hatimaye kufika kwenye ofisi za Halmashauri ya Arusha ya Meru, kujipatia fursa Mikopo ya Pembejeo zenye riba nafuu ambazo kila mkulima wa kitanzania anamudu ili kufikia malengo.
Kauli Mbiu ya Nanenane 2022 ni "AJENDA YA 10 -30 KILIMO NI BIASHARA 'SHIRIKI KUHESABIWA KWA MIPANGO BORA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI"
PICHA ZA MATUKIO
Mkurugenzi Mtndaaji Halmashaufiya Arusha Weleman Msumi,( wa kwanaa kushoto) akiwa na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri yaMeeu, Mwl. Zainabu Makwinyu, wakiwa kwenye mabanda ya Mifugo ya Halmashauri hizo.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.