• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MADIWANI ARUSHA DC WARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA MAENDELEO KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022..

Posted on: August 13th, 2022

Na Elinipa Lupembe.

Waheshimiwa Madiwani halmashauri ya Arusha wameridhishwa na  jitihada kubwa za utekelezaji wa shughuli mbalimbali na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kisekta, zilizilizofanyika kipindi cha mwaka wa fedha uliomalizika na kuishia tarehe 31 Juni 2022.

Madiwani hao wametoa pongezi hizo mara baada ya Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya hiyo, kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa mwaka wa fedha 2021/2022, wakati wa mkutano Maalumu wa mwaka wa Baraza Madiwani, uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.

Madiwani hao hawakusita kueleza hisia zao juu ya mafanikio makubwa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika halmashauri na kubainisha kuwa, kwa sasa kuna tofauti kubwa za kimaendeleo katika halmashauri hiyo tofauti na miaka iliyopita na kuipongeza serikali ya awamu ya sita.

"Tunaipongeza serikali yetu ya awamu ya sita, tunampongeza Rais wetu, Mama Samia Suluhu, kwa kutuletea fedha za nje ya bajeti kiasi cha shilingi bilini 3 za kutekeleza miradi mikubwa, miradi ambayo imekamilika kwa wakati na tayari inawahudumia wananchi" Wasema Madiwani hao

Mwenyekiyi wa halmashauri ya Arusha, Mhe.Ojung'u Salekwa, ameweka wazi kuwa halmaahauri imafanyakazi nzuri kwa mwaka uliopita na kuahidi kuongeza kasi ya usimamizi wa shughuli za maendeleo ili kugikia lengo la serikali la kuwahudumia wananchi wa halmashauri hiyo.

Diwani wa kata ya Oldonyosambu Mhe. Raymond Lairumbe amesema kuwa, amekuwepo kwenye baraza hilo tangu mwaka 2015, lakini kuna tofauti kubwa ya kimkakati utekelezaji, ambayo inafanikisha shughuli nyingi kukamilika kwa wakati na viwango huku ukusnayaji wa mapato ya halmashauri.

"Mwaka wa fedha 2021/2022, tumeendela kupata hati safi kwa miaka 6 mfululizo, tumekusanya mapato kwa asilimai 94 ambayo haijawahi kutokea, miradi mingi na mikubwa imetekelezwa na kukamilika, yatupasa tujipongeze madiwani kwa usimamizi, tuwapongeze na watalamu kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya kwa sasa" Amesisitiza Mhe. Lairumbe

Naye Diwani wa kata ya Oljoro, Mhe. Sanare Mepalary, licha ya kupongeza jitihada hizo, ametaka halamshauri kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kufikia asilimia 100 pamoja na kubuni vyanzo vipya vya mapato, vitakavyowezesha utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa uwanda mpana zaidi.

Naye Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mhe. Noah Lembris, licha ya kupongeza juhuudi za watalamu kwa kudpshirikiana na madiwani hao, amewataka kwa pamoja kusimamia miradi yankimkakati iliyoanzishwa na halmashauri hiyo, ikiwemo shule za mchepuo wa kiingereza, mashine ya kufyatulia matofali ili miradi hiyo iwe endelevu na kuipatia halmaahauri mapato, kwa kufanya hivyo fedha hizo zitaweza kupunguza changamoto za kuwahudumia wananchi kisekta.


Akiwasilisha taarifa hiyo ya mwaka mkurugenzi Msumi , amebainisha kuwa halmashauri imefanikiwa kukusanya mapato ya ndani kwa 94.9% na kutekeleza miradi ya maendeleo ya bajeti kwa asilimia 78.6 , na kutekeleza miradi ya nje ya bajeti kwa asilimia 70.8  fedha kutoka serikali kuu kupitia tozo, EP4R na UVIKO 19 huku halmashauri ikipata hati safi ya ukaguzi kwa miaka sita mfululizo.

Aidha amefafanua kuwa halmashauri imefanikwa kufanya vizuri kisekta ya Utawala jumla ya watumishi 638 walipandushwa vyeo, watumishi 545 walilipwa malimbikizo ya mishahara na watumishi 54 waliajiriwa huku sekta ya elimu ikipata ufaulu wa 100% na kushika nafasi ya kwanza kimkoa matokeo ya kidato cha sita.

Mkutano Maalum wa Baraza la Madiwani wa mwaka, umefanyika kwa mujibu wa sheria na kanuni za serikali za mitaa, ukiwa na agenda za taarifa za maendeleo za mwaka wa fedha 2021/2022, uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti, uundaji wa Kamati za Kudumu za halmashauri pamoja na uchaguzi wa wenyeviti wa kamati hizo za kudumu.


ARUSHA DC TUPO YPTAYARI KUHESABIWA

SHIRIKI SENSA YA WATU NA MAKAZI

JIANDAE KUHESABIWA 23.08.2022


PICHA ZA MATUKIO







Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.