Na Elinipa Lupembe
Madiwani halmashauri ya Arusha wameishauri Ofisi ya Mkurugenzi kushirikisha wadau wa maendeleo katika mchakato wa kuwawezesha usafiri wa pikipiki watendaii wa kata kama ilivyo adhma ya Serikali ya kuwezesha mazingira rafiki ya utawala bora kwa watumishi wa Umma ili kurahisisha ufuatiliaji na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Kata zao.
Madiwani hao wametoa ushauri huo wakati wa mkutano wa baraza la madiwani wa kuwasilisha taatifa za maendeleo ya kata kwa robo ya pili ya mwezi Oktoba – Devemba 2022 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo.
Kaimu mwenyekiti wa kikao hicho Mhe. Baraka Simon ametumia fursa hiyo kuishauri ofisi ya mkurugenzi kuwashirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo ili kuweza kufanikisha upatikanaji wa pikipiki kwa watendaji kata ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na wepesi zaidi.
“Tunatambua mchango mkubwa wa Serikali katika kuwawezesha Watumishi wetu wa Umma katika kutekeleza majukumu yao ya kuleta maendeleo katika Kata zetu, hivyo nitoe ushauri kwa ofisi ya mkurugenzi iwashirikishe na wadau wa maendeleo waweze kutusaidia katika jambo hili kwa wakati.” Ameshauri Mhe. Mesiaki.
Aidha, ushauri huo umekuja mara baada ya waheshimiwa madiwani kuhoji juu ya mpango wa Serikali wa kuboresha mazingira rafiki ya Utawala bora katika ngazi ya Kata na Vijiji ikiwemo ujenzi wa ofisi za kutolea huduma kwa kata ambazo hazina ofisi kama vile Kata ya Kiutu ambayo haina Ofisi za vijiji pamoja na changamoto ya usafiri kwa watendaji wa Kata.
“Tunaishukuru Serikali kwa kuwapatia usafiri wa pikipiki watendaji wa kata zetu, lakini tunaomba pia iendelee kutoa kipaumbele kwa watendaji wa kata zote ndani ya halmashauri yetu ili watendaji hawa weweze kutekeleza majukumu yao kwa wakati.” Amesisitiza Diwani Kata ya Oloirien Mhe. Erick Semboja.
Akijibu changamoto hiyo, kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha na Mkuu wa Kitengo Sheria Monica Mwailolo, amesema kuwa halmashauri imetenga fungu kwa bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili ya ununuzi wa pikipiki tano ili kuendelea kupunguza changamoto ya usafiri kwa watendaji wa kata.“Tunatambua kuwa changamoto hii ni kubwa kwa watendaji wetu, hivyo sisi kama halmashauri tutaendelea kutenga bajeti kila mwaka kulingana na uhitaji hadi pale changamoto hii itakapo fikia ukomo na watendaji hawa waweze kutekeleza majukumu yao kwa wepesi Zaidi.” Ameweka wazi Kaimu Mkurugenzi Mwailolo
Itakumbukwa kuwa, hivi karibuni serikali ilitoa pikipiki 197 kwa ajili ya Maafisa Watendaji wa kata nchini, halmashauri ya Arusha ikipata mgao wa pikipiki 8 na kuwa na upungufu wa pikipiki 19 kati ya kata 27 za halmashauri hiyo.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.