Na Elinipa Lupembe
Hayawi hayawi sasa yamekuwa hatimaye shilingi milioni 100 fedha za Pochi la Mama, zinategemea kukamilisha jengo la ghorofa mbili shule ya Sekondari Kiranyi, ujenzi ambao uko katika hatua za mwisho za ukamilishaji.
Kiasi hicho cha fedha kimejumuisha ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa, ofisi ya walimu, viti na meza 5 za walimu pamoja viti na meza 200 za wanafunzi, fedha kutoka Serikali Kuu, maarufu kama 'POCHI LA MAMA'.
Mkuu wa shule ya sekondari Kiranyi, Mwl. Omary Nyango, amebainisha kuwa, ujenzi wa vyumba 5, umefanikisha kukamilisha jengo la ghorofa 2 lenye jumla ya vyumba vya madarasa 18, viti na meza 450 vya wanafunzi pamoja na viti na meza 5 za walimu.
Amefafanua kuwa ukamilishaji wa jengo hilo umefanyika kwa awamu mbili ambapo mwaka wa fedha 2021/2022 serikali ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 260 na kutumika kujenga vyumba 13 vya madarasa na ofisi za walimu, zikiwa ni fedha za mapambano dhidi ya UVIKO 19.
Kwa awamu ya pili mwaka wa fedha 2022/2023 serikali ikaongeza fedha kiasi cha shilingi milioni 200 za kujenga vyumba 5 vya madarasa , madarasa ambayo yamekamilisha jengo hilo la ghorofa 2, na kufanya mazingira ya kujifunzi na kufundishia kuwa ya uhakika zaidi kwa walimu na wanafunzi.
"Jengo hili la ghorofa 2 lina jumla ya vyumba 18 vya madarasa na ofisi tatu za walimu na meza na viti, kwa pamoja vimegharimu shilingi milioni 360". Amefafanua Mkuu huyo wa shule
Ifahamike kuwa mradi huu wa ujenzi ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 - 2025 wa kuboresha miundombinu ya elimu nchini, huku zote zikiwa ni za nje ya bajeti, kwa bajeti ya halmashauri iliyoidhinishwa na Bunge kwa miaka yote hiyo miwili.
ARUSHA DC
KaziInaedelea✍✍
PICHA ZA MAENDELEO YA UJENZI WA VYUMBA 5 VYA MADARASA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.