Mama Leah Long'idu (70) amechaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa Bodi ya maji ya mamlaka ya maji Ngaramtoni (NGAUWSA), uchaguzi uliofanyika wakati wa mkutano mkuu wa kwanza wa bodi, tangu kuzinduliwa kwake, mkutano uliofanyika kwenye ofisi za NGAUWSA eneo la Ngaramtoni.
Mama Long'ido ameshinda nafasi hiyo baada ya kumshinda mgombea mwenzake kwa kupata kura tatu kati ya kura tano zilizopigwa na wajumbe halali sita wa bodi hiyo.
Akitangaza matokeo hayo, Mtendaji Mkuu Mamlaka ya mji mdogo Ngaramtoni, Sophia Shoko, amesema kuwa, Saada Msangi amepata kura 2, na Leah Long'idu amepata kura 3 kati ya kura tano zilizopigwa.
"Kwa mujibu wa sheria, kwa matokeo hayo, ninamtangaza Leah Long'idu kuwa makamu mwenyekiti wa bodi ya NGAUWSA, nafasi atakayoitumikia kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa" amesema Shoko.
Kitaaluma mama Leah Long'idu ni mwalimu, ambaye amestaafu utumishi wa umma kwa mujibu wa sheria, akiwa Mratibu wa Elimu kata ya Kiranyi halmashauri ya Arusha.
Akizungumza baada ya kutangazwa mshindi, licha ya kuwashukuru wajumbe kwa kumuamini na kumpa nafasi hiyo, Long'idu amewataka wajumbe wote kushirikiana kufanya kazi na kubuni mikakati thabiti ya kuhakikisha wananchi wa Ngaramtoni wanapata maji safi na salama sambamba na utunzaji wa mazingira hasa ya vyanzo vya maji.
Mkutano huo umetanguliwa na ziara ya wajumbe hao, ya kutembelea miradi ya maji na vituo vya kuchotea maji, kwa lengo la kujionea hali halisi ya upatikanaji wa maji katika eneo la mamlaka ya mji mdogo Ngaramtoni.
Hata hivyo wajumbe hao wa bodi wameonesha ari ya kuanza kazi kwa kasi, ili kuendandana na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya Hapa kazi tuu pamoja na kufikia lengo la serikali la kumtua mama ndoo kwa kuhakikisha huduma za maji zinapatikana kwa asilimia 95% kwenye mji wa Ngaramtoni ifikapo mwaka 2020.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.