• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MAZIWA YA MAMA MIEZI 6 YA MWANZO HUIMARISHA KINGA YA MWILI KWA MTOTO

Posted on: August 2nd, 2020

Na. Elinipa Lupembe.

   Jamii imetakiwa kuelewa kuwa, kumnyonyesha mtoto maziwa ya mama kwa miezi sita ya mwanzo bila kumpa chakula kingine, huimarisha kinga ya mwili, inayomkinga dhidi ya maradhi pamoja na kumjenga mtoto kiakili na kisaikolojia.

   Hayo yameelezwa na Mratibu wa Afya ya Uzazi, na muuguzi hospitali ya wilaya Olturumet, halmashauri ya Arusha, Butolwa Bujiku, wakati akitoa elimu ya unyonyeshaji kwa viongozi na wakazi wa kijiji cha Oltulelei kata ya Ilboru, katika shughuli za kuadhimisha ya wiki ya Unyonyeshaji Duniani 2020.

      Butolwa ameeleza kuwa, mama baada ya kujifungua, anatakiwa kumnyonyesha mtoto, kwa kipandi cha miezi sita ya mwanzo bila kumpa chakula kingine chochote, jambo ambalo linajenga  afya ya mtoto, ikiwa ni pamoja na kumjengea kinga ya mwili dhidi ya maradhi, kujenga mtoto kiakili na kisaikolojia pia.

    Amewataka wazazi kuacha tabia ya kumpa mtoto chakula kingine chochote, kwa kuwa maziwa ya mama yana lishe  na virutubisho vya kutosha kwa miezi sita ya mwanzo na kuongeza kuwa, kuanza kumpa mtoto chakula kwa kipindi hicho, huharibu mfumo mzima wa ukuaji wa mtoto, na madhara yake huonekana katika kipindi chote cha maisha yake.

       "Kuanza kumpa mtoto chakula kabla ya kufikisha miezi sita, kuna madhara makubwa kwa mtoto, huaribu mfumo wa mzima wa ukuaji wa mtoto, huchosha utumbo na mfumo wa mmeng'enyo, huleta udumavu wa mwili na akili na humuathiri mtoto kisaikolojia, ni vema kuzingatia unyonyeshaji wa maziwa ya mama kwa miezi sita ya mwanzo ili kuepuka madhara hayo kwa mtoto" amesisitiza Mratibu huyo.

       Naye Afisa Lishe Halmashauri ya Arusha, Doto Milembe amewaondoa wasiwasi watu wanadhani maziwa ya mama peke yake, hayatoshi kwa lishe ya mtoto na kusisitiza kuwa, maziwa yhayo yana virutubisho vya kutosha kwa mtoto wa chini ya miezi sita, yakiwa na viini lishe vya makundi yote ya vyakula pamoja na maji.

    Aidha ameitaka jamii kufahamu kuwa, jukumu la unyonyeshaji mtoto si la  mama peke yake bali ni jukumu la familia na jamii kwa ujumla ili kuwa na kizazi chenye afya bora kwa maendeleo ya familia, jamii na Taifa.

     Hata hivyo viongozi wa kijiji cha Oltulelei, wamekiri kuridhishwa na mafunzo hayo, kwani yamewapa uelewa mkubwa juu ya umuhimu wa kumnyonyeshaji mtoto kwa miezi sita ya mwanzo, jambo ambalo hapo awali hawakufahamu umuhimu wake kwa kina na kuomba elimu hiyo itolewe kwa jamii nzima ili kuwa na watoto wenye afya bora kwa maendeleo ya Taifa lao.

"Tumerishwa na mafunzo haya, yametuondoa gizani kwani wengi tulidhani haiwezekani maziwa ya mama kumtosheleza mtoto, kumbe maziwa ya mama yanatosha na yana virutubisho vyote katika makundi yote ya vyakula" wamesema viongozi hao.

   Tatu Shabani mkazi wa kitongoji cha Oltulele amekiri kuwa, licha ya kuwa yeye ni mama mwenye watoto lakini hakufahamu sana, madhara yanayotokana na kuanza kumpa mtoto chakula kabla ya kufikisha miezi sita, na kukiri kuanza kutumia maarifa hayo na kuendelea kuitoa elimu hiyo kwa watu wanomzunguka.

       Halmashauri ya Arusha, imeungana na mataifa mengine duniani, kuadhimisha wiki ya unyonyeshaji Duniani 2020, kwa kutoa elimu na kuhamasisha jamii umuhimu wa mama kunyonyesha mtoto kwa miezi sita ya mwanzo bila kumpa kitu chochote na kumnyonyesha kwa siku 1000.

   "Maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji Duniani 2020, yamebeba Kauli Mbiu ya Sote kwa pamoja: Tuwawezeshe wanawake Kunyonyesha kwa Afya Bora na Utunzaji wa Mazingira"


Mratibu wa Afya ya Uzazi halmashauri ya Arusha, Butolwa Bujiku akitoa elimu ya unyonyshaji kwa viongozi wa Kitongoji cha Oltulele kata ya Ilboro ikiwa ni Maadhimisho ya Wiki ya Unyonyeshaji, halmashauri ya Arusha.


Viongozi wa Kitongoji cha Oltulele kata ya Iboru wakifuatilia mijadala ya elimu ya unyonyeshaji.






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.