Na Elinipa Lupembe
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, Mhe. Noah Lembris amesema kuwa katika kipindi cha awamu ya sita, Jimbo lake limepata fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo tofauti na awamu zilizotangulia.
Mhe. Noah ameyasema hayo wakati akitoa salamu kwa wananchi waliohudhuria hafla fupi ya makabidhiano ya mradi wa ujenzi wa vyumba 38 vya madarasa halmashauri ya Arusha, hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Mringa.
Mbunge huyo ameeleza mafanikio ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo Jimbo hilo la Arumeru Magharibi limepata fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo katika sekta za Elimu, Afya, maji na miundombinu ya barabara, miradi ambayo imeondoa kero zilizokuwa zikiwakabili wananchi wa jimbo hilo kwa muda mrefu.
Amesema kuwa licha ya kuwa mwaka 2022 serikali imetoa shilingi Milioni 760 za kujenga madarasa 38 kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2023, amebainisha kuwa fedha hizo ni sehemu ndogo ya fedha ambazo serikali ya awamu ya sita imezitoa jimboni humo.
"Milioni 760 ni sehemu tuu ya miradi iliyotekelezwa na Serikali ya CCM ndani ya ndani ya Jimbo hili, lakini serikali imetoa shilingi Bilioni 22 za ujenzi wa barabara yenye urefu wa Km 18 ya kutoka Mianzini, Timbolo, Sambasha mpaka Ngaramtoni, yote hayo ni mafanikio makubwa ndani ya Jimbo letu la Arumeru Magharibi kwa muda mfupi sana". Ameweka wazi Mhe. Noah.
Ameongeza kuwa wananchi wa Arumeru Magharibi wana kila sababu ya kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa miradi mingi ya maendeleo ambayo inatatua kero na changamoto nyingi katika hizo sambamba na kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi.
Aidha hakusita kuwawapongeza watendaji wote kuanzia ngazi ya wilaya, halmashauri na kata na shule kwa kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa ubora kwa kuzingatia viwango vinavyoendana na thamani ya fedha zilizotolewa na serikali 'value for money'.
ARUSHA DC
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.