Na Elinipa Lupembe.
Mkuu wa shule ya sekondari Losinoni, Mwl. Emmanuel Mkonongo, Halmashauri ya Arusha, akiwasilisha mada juu Mapambano dhidi ya ujinga kwa miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika.
Mwl, Mkonongo ameeleza namna serikali ilivyopambana kuhakikisha wananchi wake wanafuta kuzitaifisha shule zilizokuwa zinamilikiwa na wakoloni na kuendeshwa na serikali.
kupitia shule hizo, asilimia kubwa ya watanzania sasa wamepata nafasi ya kupata elimu kuanzia elimu ya awali mpaka chuo kikuu, juhudi ambazo zimewezesha nchi kupata watalamu wa fani mbalimbali ndani ya nchi, tofauti na hapo awali serikali ilitumia watalamu kutoka nje ya nchi kutokana na kukosekana wasomi wazawa.
"Kwa sasa Serikali imetoa fursa kwa kila mtanzania kuwa na haki ya kupata elimu, kuanzia elimu ya awali mpaka chuo, kikuu, tofauti kabla ya Uhuru elimu ilitolewa kwa ubaguzi, lakini zaidi uwepo wa shule za serikali kila kata na zile za maahirika ya dini sambamba na shule binafsi kwa ujumla zimetoa wigo wa wananchi kuondokana na ujinga"
Baada ya Uhuru serikali ilijikita kwa wananchi wake kufuata ujinga kwa kuhakikisha wananchi wanajifunza Kusoma, Kuandika na kuhesabu, kwa sasa Taifa linatafuta wasomi wataalam wa fani mbalimbali na si wasomo wa KKK tatu.
Kumekuwa na maendeleo makubwa katika kupambana na ujinga hali iliyowawezesha watanzania kupambana na maadui umaskini na maradhi pamoja na kujikomboa kiuchumi, kiutamaduni na kajamii, mambo yaliyofanya maendeleo makubwa ya watanzania kwa sasa.
Mdahalo uliojumisha wananchi wa halmashauri ya Arusha kujadili mada ya "MIAKA 61 YA UHURU NA MAPAMBANO DHIDI YA MAADUI UJINGA, UMASKINI NA MARADHI". ukiongozwa na Katibu Tawala Wilaya ya Arumeru Mwl. James Mchembe kwenye ukumbi wa shule ya Msingi Green Acres eneo la Sekei.
Mdahalo huo ikiwa ni maalum kuelekea maadhimisho ya sikuu ya Uhuru wa Tanganyika tarehe 09.12.2022.
ARUSHA DC
KaziInaendelea✍✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.