Na Elinipa Lupembe - ARUSHA DC
Kuelekea maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika, wananchi halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru wamekiri kuwepo mafanikio makubwa nchinim katika sekta za elimu, uchumi na afya, yaliyotokana na juhudi za serikali za mapambano dhidi ya maadui ujinga, umaskini na maradhi.
Wananchi hao wamedhibitisha hayo, wakati wa Mdahalo maalum uliowashirikisha wakazi wa halmashauri ya Arusha, uliobeba mada ya "Miaka 61 ya Uhuru na Mapambano dhidi ya maadui Ujinga, Umaskini na Maradhi".
Mdahalo huo uliongozwa na Katibu Tawala Wilaya ya Arumeru Mwl. James Mchembe, wananchi wamebainisha matokeo ya mapambano dhidi ya ujinga yanayojidhihirisha wazi, kutokana na ongezeko la wasomi lililotokana na uwepo wa shule na vyuo vya kati na vikuu katika mikoa yote nchini, uliotoa fursa ya kila mtanzania kupata elimu.
"Kwa sasa Serikali imetoa fursa kila mtanzania kuwa na haki ya kupata elimu, kuanzia elimu ya awali mpaka chuo kikuu, tofauti kabla ya Uhuru elimu ilitolewa kwa ubaguzi, kubwa zaidi uwepo wa shule za serikali kila kata, za mashirika na binafsi kwa ujumla zimepanua wigo wa wananchi kuondokana na ujinga" Mwl. Emanuel Mkonongo.
Ameongeza kuwa baada ya Uhuru serikali ilijikita kwa wananchi wake kufuata ujinga kwa kuhakikisha wananchi wanajifunza Kusoma, Kuandika na kuhesabu, kwa sasa Taifa linatafuta wasomi wataalam wa fani mbalimbali na si wasomo wa KKK tatu.
Bw. James Magumba amezungumzia hali halisi ya mabadiliko katika sekta ya usafiri na usafirishaji, watanzania wakiwa wanajivunia maendeleo ya miundombinu ya barabara zinazofikika katika mikoa yote Tanzania hadi katika maeneo ya vijijini.
"Kwa sasa watanzania tunasafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi, bila ya kuwa na kikwazo, tofauti kubwa baada ya Uhuru mtu alisafiri zaidi ya siku 4 sehemu ya kufika kwa siku moja, Mungu ibariki Tanzania" Amebainisha Bw. Magumba
Victo Karia amezungumzia mabadiliko katika sekta ya afya kuanzia mtu binafsi, upatikanaji wa huduma za afya, uwezeshwaji wa upatatikanaji wa huduma za afya pamoja na ushirikishwaji wa jamii katika kupambana na magonjwa kupitia watoa huduma ngazi ya jamii.
Bw. Karia amebainisha mabadiliko ya kiafya yaliyotokana na mapambano dhidi ya ujinga na umaskini yaliyomuwezesha mtanzania mwenyewe kufahamu namna ya kujikinga na maradhi kupitia lishe bora na usafi wa mtu na mazingira, jambo ambalo zamani watu wengi walipoteza maisha kutokana na magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu, surua, utapiamlo magonjwa ambayo watanzania wa sasa wamefahamu namna ya kujikinga.
Serikali imefanikiwa kuboresha sekta ya afya kwa kusogeza huduma za afya, karibu na wananchi kwa kuhakikusha kila kijiji kina zahanati, kata ina kituo cha afya, hosptali ya wilaya na kuwa hosptali za rufaa za mkoa, jambo ambalo licha ya kurahisisha upatikanaji wa matibabu, limeondoa msongamano hospitalini.
Mdahalo ni maalum kuelekea maadhimisho ya sikuu ya Uhuru wa Tanganyika tarehe 09.12.2022.uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano shule ya Msingi Green Acres kata ya Kikata
yARUSHA DC
KaziIendelee✍✍
PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA MDAHALO
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.