• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Migogoro ya ardhi yatajwa chanzo cha hasara kwa jamii

Posted on: March 15th, 2018

Kufuatia migogoro ya ardhi inayotokana na matumizi yasiyo rasmi na kusababisha hasara kwa jamii na taifa, Tume ya taifa ya kupanga matumizi bora ya ardhi imeanza kuwajengea uwezo watalamu wa halmashauri juu ya matumizi bora ya ardhi kwenye ngazi za vijiji.

Baada ya kujengewa uwezo, watalamu hao watakwenda kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi kwenye vijiji vyote ndani ya halmashauri ya Arusha ili kuwa na ardhi bora iliyopangwa na kutunzwa kulingana mahitaji ya jamii husika.

Mkurugenzi msaidizi Tume ya taifa ya kupanga matumizi bora ya ardhi, Albina Bura amesema kuwa suala la kupanga ardhi ni suala mtambuka linahitaji ushirikishwaji wa watalamu fani mbalimbali watakaowezesha kupanga ardhi kulingana na matumizi ya eneo husika na uhitaji wa jamii.

Amesisitiza kuwa mipango bora, ya matumizi bora ya ardhi, yanatakiwa kuanzia ngazi ya vijiji kule ambako bado ardhi haijavamiwa kwa kiasi kikubwa.

Ameongeza kuwa kutokana na ongezeko la watu linalosababisha uhitaji mkubwa ardhi, ardhi inatakiwa kutunzwa na kupangwa kwa ajili ya vizazi vijavyo kwa kuwa ardhi haiongezeki.

"Ni vema kupanga matumizi bora ya ardhi vijijini, ili ardhi hiyo iweze kutumika kwa wakazi wote kulingana na shughuli halisi za jamii bila kuathiri mazingira" amesema Bura

Aidha ameongeza kuwa jamii inapaswa kukubali kutumia ardhi kulingana na mipango ya matumizi ya ardhi, mipango itakayoandaliwa kitaalamu kulingana na mahitaji ya jamii husika.

Bura amezitaka halmashauri kuanza kupanga ardhi kwenye vijiji ambavyo ukuaji wake unadalili za kuwa miji ili jamii ikute tayari kuna mpango wa matumizi bora ya ardhi hiyo.

Afisa Mifugo halmashauri ya Arusha Epifania Swai amesema kuwa kuna bado kuna tatizo la wafugaji kufuga mifugo mingi kuliko eneo, jambo linalosababisha uharibifu wa mazingira hasa ardhi na kuongeza kuwa kupitia mafunzo hayo halmashauri itaendelea kuhamasisha na kutoa elimu zaidi kwa jamii ya wafugaji ili waweze kupunguza mifugo na badala yake kufuga mifugo michache yenye tija.

Naye Afisa Kilimo, Elisha Sanari amesema kuwa mpango bora wa ardhi utawezesha kutumia ardhi ndogo kulima, kufuga na hata makazi tofauti na sasa kilimo na mifugo vinafanyika bila mpango.

Hata hivyo jamii inapaswa kufahamu kuwa ardhi ni rasilimali yenye thamani kubwa na isiyoongezeka licha ya kuwa watu wanaongezeka na wanahitaji kutumia ardhi hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.