• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MILIONI 200 ZA EP4R ZAKARABATI MABWENI SHULE YA SEKONDARI ILBORU.

Posted on: September 7th, 2022

Na Elinipa Lupembe


Kufuatia mpango mkakati wa serikali wa kuboresha miundombinu ya elimu hususani kwenye shule kongwe nchini, wizara ya Elimu kupitia mradi wa EP4R imetoa fedha, kiasi cha shilingi milioni 200 kwa ajli ya ukarabati wa mabweni shule ya sekondari Ilboru, halmashauri ya Arusha.

Akizungumza wakati wa kukagua maendeleo ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amethibitisha mapokezi ya kiasi hicho cha fedha kutoka Serikali kuu, kwa ajili ya ukarabati wa mabweni manne shule ya sekondari Ilboru na tayari utekelezaji wa mradi huo unaendelea na uko katika hatua za mwisho za ukamilishaji.

Aidha ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha, kwa kuwa mabweni ya shule hiyo yalikuwa kwenye hali ya uchakavu  uliotokana na kujengwa zaidi ya miaka 50 iliyopita.

"Tumenza mwaka mpya wa fedha 2022/2023 vizuri, mwishoni mwa mwezi Julai tumepokea fedha hizo za ukarabati wa mabweni ya shule yetu kongwe ya Ilboru, ukarabati huu utawezesha wanafunzi kulala kwenye mazingira rafiki". Amefafanua Mkurugenzi Maumi

Naye Mkuu wa Shule ya sekondari Ilboru, Mwl. Denis Otieno, amebainisha kuwa fedha hizo zimekuja wakati muafaka kwa kuwa  mabweni hayo yalikuwa yamechaka, ukarabati huu ni wa msingi sana kwa  wanafunzi na shule kwa ujumla wake.

"Mabweni yalikuwa yamechoka, yalijengwa mwaka 1963, ukarabati huu, utawezsha watoto kulala kwenye mazingira safi na rafiki, jambo ambalo tunaamini litakuwa na matokeo makubwa kitaaluma katika shule yetu" Amesema Mkuu huyo wa shule.

Aidha amefafanua kuwa, fedha hizo kiasi cha shilingi milioni 200, zinatumika kukarabati mabweni manne, ikiwemo kubadilisha mapaa, kubadilisha mifumo ya maji safi na maji taka, mfumo wa umeme, kubadilisha milango, madirisha na vioo vya madirisha, kukarabati vyoo,  kuziba nyufa pamoja na kupaka rangi ndani na nje ya majengo hayo.

"Tunaishukuru serikali kwa kuwa mabweni yote manne yanalaza jumla ya wanafunzi 760, huku kila bweni likilaza wanafunzi 190, kwa mazingira bora ya kulala ni uhakika wa afya za wanafunzi na taaluma" Amefafanua Mkuu huyo wa shule

Ifahamike kuwa shule ya sekondari Ilboru ni shule ya wavulana na ni  miongoni mwa shule kongwe nchini, yenye jumla ya wanafunzi 860, inayofanya vizuri kitaaluma kwa kushika nafasi 10 bora kitaifa kwa matokeo ya mitihani ya Taifa ya kidato cha nne na cha sita.


ARUSHA DC

TUPO KAZINI✍✍















Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • DKT. PASCAL KATIKA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 19, 2025
  • WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

    June 18, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI

    June 17, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.