• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKULIMA LOMAYANI APATA KOMBE LA MKULIMA BORA MKOA WA ARUSHA

Posted on: August 8th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Mkulima Isaya Lomayani  kutoka Kata ya Mwadent, halmashauri ya Arusha, amekuwa mkulima bora kwa kushika nafasi ya kwanza kwa mkoa wa  Arusha, kwenye maonesho ya Nanenane kanda ya Kaskazini yanayofanyika kwenye viwanja vya nanenane eneo la  Themi -Njiro Jijini Arusha.

Isaya Lomayani amekabidhiwa kombe kubwa na Mgeni rasmi wakati wa kufunga maonesho hayo,  mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Makongoro Nyerere, mara baada ya kuwabwaga wakulima kutoka halmasahuri zote saba za mkoa wa Arusha

Mkulima Lomayani anayejihusisha zaidi na kilimo cha mboga mboga na mahindi, amekiri kilimo hicho kumuingizia kipato kutokana na kufuatilia maelekezo anayopatiwa na watalamu wa halmashauri ya Arusha sambamba na kumuunganisha na wadau na makampuni yanayojihusisha na mbegu bora na masoko.

"Ninalima mbogamboa na mahindi, kilimo ambacho nimekiboresha miaka ya hivi karibuni na kukifanya kilimo biashara, mara baada ya kupata mafunzo ya teknolojia ya uzalishaji bora kutoka kwa mtalamu wa kilimo kwenye kata yangu ya Mwandet kwa kushirikiana na wadau wengine wa kilimo" Amefafanua Lomayani

Lomayani licha ya kuushukuru uongozi wa mkoa wa Arusha na waandaaji wa Maonesho hayo, ameweka wazi kuwa maonyesho ya nanenane yanawapa nguvu wakulima na wafugaji ya kujiona kuwa nao ni sehemu ya mafanikio ya serikali ya Tanzania.

Hata hivyo mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi, licha ya kumpongeza mkulima huyo, amewashukuru wakulima, wafugaji na wadau wote wa halmasahuri hiyo, walioshiriki kwenye maonesho ya nanenane 2022, hata kama hawakuwa washindi wameonyesha uzalendo wa hali ya juu kwa kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta ya Kilimo na mifugo.

Aidha Mkurugenzi Msumi amewataka wakulima na wafugaji, kuwatumia Maafisa Ugani walio katika maeneo yao, kupata utaalmau sambamba na kujifunza teknolojia za kilimo cha kisasa ikiwa ni mkakati wa halmashauri kufikia Ajenda 10 - 30 ya Kilimo Biashara.

Kauli mbiu ya maonyesho ya Nanena 2022 ni Ajenda 10-30 Kilimo Biashara; Shiriki Sensa ya Watu na Makazi kwa Mipango Bora ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.


PICHA ZA MATUKIO

Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Makongoro Nyerere akimkabidhi kombe la Mshindi wa kwanza mkulima bora mkoa wa Arusha Isaya Lomayani, mara baada ya kufunga maonesho ya nanenane 2022 kanda ya Kaskazini, kwenye viwanja vya Themi -Njiro jijini Arusha.



Mkulima wa Kata ya Mwandet halmashauri ya Arusha, Isaya Lomayani akiwa ameshikilia kombe la ushindi wa Mkulima bora Mkoa wa Arusha mara baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Makongoro Nyerere.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akiwa ameshikilia kombe la ushindi wa Mkulima bora Mkoa wa Arusha Isaya Lomayan, mara baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Makongoro Nyerere.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha, Seleman Msumi akiwa kwenye picha ya pamoja na wakulima walioshiriki maonyesho ya nanenane kwenye banda la kilimo la halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.