Baada ya Watalamu wa halmashauri ya Arusha, wataalamu Washauri wa kampuni ya Don Consult Ltd kufanya kikao na viongozi wa serikali, wazee wa mila na koo, watu mashuhuri na wawakilishi wa wananchi wa kijiji cha LENGIJAVE kata ya OLKOKOLA wiki iliyopita wamefanyika mkutano mkuu wa kijiji ulioshirikisha wananchi wote wa vitongoji vyote vya kijiji hicho kwa lengo la kuutambulisha mradi wa maji wa WaterAid ambao uko katika hatua za awali za utekelezaji utakatekelezwa kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2017 mpaka Mei 2018.
Tofauti na maeneo mengine wananchi wa Lengijave walionyesha furaha na hamu kubwa ya kuupokea mradi huo kutokana na adha kubwa wanayoipata kutokana na shida kubwa ya maji inayowakabili wananchi hao kwa pamoja wamekubali kiupokea mradi huo kwa moyo mmoja na kukubali kutoa ushirikiano wa hali na mali wakati wote wa utekelezaji wa mradi huo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Lengijave ambaye ndiye Diwani wa kata ya Olkokola mheshimiwa Kalanga amewahakikishia wataalamu hao kutoa ushirikiano wa hali ya juu kutokana na kuwa wananchi wake wana kiu ya maji na si vinginevyo.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.