• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA WILAYA YA ARUMERU MHE. AMIR MOHAMED MKALIPA AWATAKA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAFIKA SHULENI IFIKAPO TAREHE 13 JANUARI 2025

Posted on: January 11th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Mhe.Amir Mohammed Mkalipa ameawata Wazazi wote ndani ya Wilaya ya Arumeru kuhakikisha ifikapo tarehe 13/01/2025 watoto wote wanaopaswa kwenda shule wawe wamefanya hivyo kinyume chake watachukuliwa hatua za kisheria.

Hayo ameyazungumza leo tarehe 11/01/2025 katika Kijiji cha Loovilukunyi Kata ya Kisongo katika Halmashauri ya Wilaya Arusha mara baada ya kukagua ukamilishwaji wa majengo ya shule mpya yaSekondari Loovilukunyi na kisha kuzungumza na Wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanika shule hapo.

Mhe,Mkalipa amesema suala la Elimu kwa watoto ni la lazima na Serikali inayoongozwa na Rais Dkt.Samia imeshaweka miundombinu vizuri ili kuwawezesha watoto kupata elimu ya msingi mpaka sekondari bure,na kuongeza kuwa Serikali haitasita kumchukulia hatua mzazi au Kiongozi wa Kijiji,Mtaa au Kata atakayeshindwa kusimamia suala la mtoto kujiunga na masomo kwa kigezo cha kuolewa.


" Niseme tu,hatutamfumbia macho mtu yeyote atakaye leta uzembe wa kutopeleka mtoto shule eti kwa kisingizuo ameshindwa kumpa mahitaji ya sare,daftari na chakula kwani gharama kubwa imebebwa na Serikali" alisema Mhe.Mkalipa.

Katika kuhakikisha suala la wanafunzi waliopangwa wanajisajili kuanza masomo siku ya tarehe 13/01/2025, Mhe.Mkalipa amemwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha Maafisa Elimu na Walimu wanaandaa taarifa ya hali ya kujisajili kwa wanafunzi hao wa shule za awali,msingi na sekondari na kuiwasilisha kwake.

Kwa upande wake,Diwani wa Kata hiyo ya Kisongo Mhe.Godson Lotha Loning'o amemshukuru Mhe.Rais Dkt.Samia kwa kutoa shilingi milioni 584 kwaajili ya ujenzi wa vyumba 8 vya madarasa,maabara pamoja na matundu ya vyoo ambapo uwepo wa shule hiyo mpya utapunguza umbali ambao watoto waliokuwa wakiutumia kwa siku ili kufuata elimu.


Shule ya sekondari Loovilukunyi ni shule mpya iliyojengwa kwa lengo la kuwapunguzia umbali mrefu watoto wa jamii ya kifugaji waliokuwa wanatumia kutafuta elimu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.