• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

MRADI WA BINTI NA MAENDELEO WALETA MAPINDUZI MUSA, WAEPUSHA WASICHANA NA NDOA ZA UTOTONI

Posted on: April 9th, 2022

Na. Elinipa Lupembe.

Mradi wa Binti na Maendeleo unaotekelezwa na Shirika la DSW Tanzania,  umefanikiwa kuzui ndoa za utotoni kwa wasichana waliokuwa wamechumbiwa tayari kuolewa, kwa kuwafanya wasichana hao, kukataa kukatisha masomo yao na kuolewa badala yake kuendelea na masomo yao, mrafi unatekelezwa kupitia vikundi vya uelimishaji rika pamoja na klabu za wapinga ukatili ndani ya shule za msingi.

Hayo yamewekwa wazi wakati wa mdahalo, uliohusisha wawakilishi kutoka makundi mbalimbali ya kijamii, wakati wa Bonanza maalum la Binti na Maendeleo, liliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingi Musa kata ya Musa, halmashauri ya Arusha, Bonanza lenye lengo la kupaza sauti ya kuelimisha jamii juu ya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Wakizungumza wakati wa mdahalo huo, kwa pamoja wameupongeza Mradi wa Binti na Maendeleo, mradi ambao wamethibitisha kuleta mapinduzi makubwa kwa kuwajengea uwezo wa kufahamu na kutambua, uhalisia wa suala zima la ukatili wa kijinsia, husani ukeketaji na ndoa za utoto pamoja na madhara yake, ukatili ambao ulikuwa ukifanyika katika maeneo hayo kutokana na mila na desturi za kabila la kimaasai, ambazo wanadai wao wamerithi kutoka kwa wazazi  na mababu zao.

"Kupitia elimu inayotolewa na vijana waelimisha rika walio nje ya mfumo rasmi wa elimu, na klabu za watoto shule ya msingi Olchoruvus, jamii yetu ya Musa sasa imepata kufahamu  madhara ya ukeketaji na kuanza kuachana na mila hiyo na zaidi jamii imetambua umuhimu wa kuwasomesha watoto wa kike, watoto ambao hapo awali walikatishwa masomo na wazazi wao na kulazimika kuolewa katika umri mdoago" wamesisitiza Wanajamii ya Musa

Hosiana Rafael mwanafunzi wa shule ya msingi Olchorovus, amebainisha kuwa, kupitia klabu yao ya Binti na Maendeleo shuleni, imefanikiwa kuwaelimisha wanafunzi wenzao kupinga na kupambana ukeketaji pamoja na ndoa za utotoni na kuongeza kuwa, elimu hiyo imefanikisha baadhi ya wasichana waliochumbiwa wameweza kuzungumza na wazazi wao na kukata kuolewa na kuamua kuendelea na masomo yao na wazazi wao wamewakubalia.

"Tunashukuru kwa sasa wazazi wetu wameanza kutuelewa, wengi wameanza kutambua madhara ya ukeketaji, na wazazi wengi sasa wameacha kuwaozesha watoto wao wakiwa shule na kuamua kuwaacha waendelee na masomo, na mpaka sasa wasichana hao  wapo shuleni, DSW imetuletea ukombozi hasa kwa wasichana wa kata ya Musa" ameweka wazi mwanafunzi Hosiana 

Mgeni rasmi katika Bonaza hilo, Afisa Maendelo ya Jamii, Ofisi ya Mkuu wa mkoa Arusha Erena Materu, licha ya kulishukuru shirika la DSW kwa kazi kubwa wanayoifanya kwa jamii, amewapongeza kwa kuungana na serikali kupambana na ukatili wa kijinsia hususani kwa wanawake na watoto, kazi ambayo ni mkakati wa serikali ya awamu ya sita sambamba na utekeleza wa Ilani ya CCM mbacho ni chama tawala.

Aidha ameipongeza jamii ya watu wa Musa kwa kupokea na kuyatumia maarifa waliyopata na kuwataka kutumia maarifa hayo, kuendelea kuelimishana wao kwa wao, ili jamii nzima ipate uelewa wa pamoja wa kutokomeza mila potofu, mila ambazo zina madhara makubwa kisaikolojia, kijamii na kiuchumi, na kusisitiza kuwa Arusha bila Ukatili inawezekana.

"Haya mambo mazuri tuliyofundishwa na DSW, tuyaendeleze na  kuyafanyia kazi kwa kuelemisha wenzetu kwa nguvu moja, tukiungana kwa pamoja kupinga ukatili katika jamii zetu, viongozi wa mila na dini wakisema, viongozi  wa  serikali na wale vyama vya siasa nao wakisema, baba na mama wakisema, vijana wa kike na wakiume wakisema, watoto wakisema, ninaamini ukeketaji na ndoa za utotoni zitakwisha na kubaki na jamii huru yenye  maamuzi sahihi kwa maendeleo ya taifa letu" amesisitiza Elena.

Mratibu wa Mradi wa Binti na Maendeleo shirika la DWS Tanzania, Juliana Mndanga, ameeleza lengo la Bonanza hilo ni kuwakutanisha pamoja, watu wa makundi na mitazamo tofauti, ili kuelemisha na kuwahamasisha kupinga ukatili wa kijinsia kwa sauti moja, kupitia shughuli za kiamii ikiwemo burudani za sanaa za ngoma na nyimbo,  michezo, jumbe mbalimbali pamoja na midhalo.

"Kupitia Bonanza hili jamii imeweza kufahamu kuwa jamii yao, inakabiliwa na  changamoto ya ukatili wa kijinsia, ukeketaji na ndoa za utotoni, kupitia shughuli mbalimbali zinazofanyika kwenye Bonanza, zinawezesha kutambua madhara ya matukio hayo ya ukatili na namna ya kuyapinga na kuyatokomeza kabisa, huku jamii ikitakiwa kutambua kiwa wakiwapa nafasi wasichana wanawaweza"  amesisitiza Juliana.

Hata hivyo Mratibu huyo wa mradi ameweka wazi kuwa, DSW kwa kushirikiana na halmashauri ya Arusha inatekeleza mradi wa Mradi wa Binti na Maendeleo kwenye shule za msingi ndani ya kata tano za Musa, Mwandet, Olmotony, Ng'iresi na Sokon II, huku kukiwa na klabu za kupinga ukatili shuleni na vijana waelimisha rika walio nje ya mfumo rasmiwa elimu.  

ARUSHA DC 

KaziIendelee✍✍



Mgeni rasmi, Afisa Maendeleo ya Jamii na Mratibu wa masuala ya ukatili wa Kijinsia, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha, Erena Materu, akizungumza na hadhara ya wananchi wa kata ya Musa,,kwenye Bonanza la Binti na Maendeleo, lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Musa na kuratibiwa na shirika la DSW.


Wawakilishi kutoka makundi mbalimbali ya kijamii, wakiwa kwenye Mdahalo  wa nini kifanyike kutokomeza Ukatili wa Kijinsia, kwenye kata yao ya Musa, wakati wa Bonanza la Binti na Maendeleo, lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Musa na kuratibiwa na shirika la DSW.

Wasichana wa rika tofauti, wakiwa kwenye Bonzanza la Binti na Maendeleo, lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Musa na kuratibiwa na shirika la DSW


Wasichana wa shule ya Msingi Musa, wakiwa na bango lenye ujumbe 'Ukatili wa Kijinsia Hamuachi mtu Salama' kwenye Bonzanza la Binti na Maendeleo, lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Musa na kuratibiwa na shirika la DSW

Mkurugenzi shirika la DSW, Peter Owaga, akizungumza na hadhara ya wananchi wa kata ya Musa, kwenye Bonanza la Binti na Maendeleo, lililofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Musa na kuratibiwa na shirika la hilo la DSW.

Afisa Mtendaji kata ya Musa, Yustina Mugera akipokea ngao kutoka shirika la DSW, ikiwa ni ishara ya utekelezaji imara wa Mradi wa Binti na Maendleo, unaohusika na kupinga ukatili wa kijinsia hususani ukeketaji na ndoa za utotoni, mradi unaotekelezwa katika kata ya Musa, na tayari matokeo yake yamenaza kuzaa matunda kwa jamii ya wana Musa.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.