• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Msamaria mwema Michael Fortson, atoa msaada wa vifaa maalum vya walemavu wa ngozi Arusha DC

Posted on: April 10th, 2018

Msamaria mwema na mwanzilishi wa shirika la kulelea watoto yatima la Neema Village, bwana Michael Fortson ametoa msaada wa vifaa maalum kwa ajilili ya walemavu wa ngozi, katika halmashauri ya Arusha.    

Bwana Fortson ametoa msaada kwa walemavu hao wa ngozi baada ya kuona jinsi walemavu hao wanavyopata shida ya ngozi kwa kukosa mafuta hayo maalumu kwa ngozi zao.  

Fortson amemkabidhi jumla ya chupa 71 za mafuta ya kujipaka, miwani 48 na kofia 48 kwa uongozi wa halmashauri huyo ili waweze kugawa vifaa hivyo,kwa walemavu hao ndani ya halmashauri.   

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Fortson amesema kuwa, anatambua madhara wanayoyapata walemavu wa ngozi endapo watakosa vifaa maalumu vya kujikinga na jua kama miwani, kofia na mafuta.      

Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo, Afisa Ustawi wa Jamii halmashauri ya Arusha, Beatrice Tengi amemshukuru bwana Fortson kwa kuunga mkono serikali ambayo kimsingi ndio imebeba jukumu hilo kubwa la kugharami vifaa vya walemavu wa ngozi, hasa wale wasio na uwezo.     

Tengi amefafanua kuwa, walemavu wengi wa ngozi hushindwa kumudu gharama za kununua vifaa hivyo, kwa kuwa huuzwa kwa bei ghali kiasi cha mtu wa kawaida kushindwa kununua.             

Ameongeza kuwa, kutokana na ufinyu wa bajeti halmashauri hutoa mafuta mara moja kwa mwaka , jambo ambalo husababisha wakati mwingine baadhi ya walema kuishi bila kupaka mafuta hayo maalumu, jambo ambalo linaweza kuwasababishia madhara.       

" Baadhi ya walemavu wa ngozi hutegemea mafuta tunayowagawia kama halmashauri, ambayo tunayatoa mara moja kwa mwaka huku walemavu hao hutakiwa kutumia mafuta hayo siku zote za maisha yao"  amesema Tengi.   

Aidha Afisa Ustawi huyo, amewaomba wadau mbalimbali, kujitokeza kuwasaidia walemavu hao wa ngozi, kutokana na ukweli kwamba, wanahitaji misaada ya vifaa kwa kuzingatia hasa wengi wao wana hali duni za kimaisha.   

Hata hivyo Tengi amethibitisha kuwa, tayari wameshaanza kuvigawa vifaa hivyo kwa wahusika, kila wanapokwenda kwenye kata na vijiji kikazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.