Na. Elinipa Lupembe.
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi, Saad Mtambule amekabidhi tena, fomu za Uteuzi wa Ubunge Jimbo la Arumeru Magharibi Bw. Hezron Kijangwa Kingazi wa Chama cha DEMOKRASIA MAKINI.
Mgombea huyo, aliwasili kwenye Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi eneo la Sekei majira ya mchana na kukabidhiwa fomu hizo za Uteuzi mnamo saa 07:59 mchana.
Aidha Msimamizi huyo wa Uchaguzi, amekabidhi fomu ya Uteuzi mgombea huyo, kufuatia Maelekezo ya Fomu ya Uteuzi Na. 8B, kwa mujibu wa Kifungu cha 38 (3) na (4) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343 ikiweka wazi mambo yaliyojumuishwa kwenye fomu ya Uteuzi.
Baada ya kuchukua fomu ya Uteuzi, Mgombea huyo amefikisha idadi ya Wagombe wanne kutoka vyama vinne vya siasa, kuchukua fomu za Uteuzi wa Ubunge kwa Jimbo la Arumeru Magharibi.
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi, Saad Mtambule (kulia), akimkabidhi fomu ya Uteuzi wa Ubunge Jimbo la Arumeru Magharibi Bw. Hezron Kijangwa Kijazi kugombea nafasi ya Ubunge kupitia Chama chaDEMOKRASIA MAKINI.
Bw. Hezro Kijangwa Kijazi akisaini daftari la kukiri kupokea fomu ya Uteuzi wa Ubunge kupitia Chama cha DEMOKRASIA MAKINI, mara baada ya kukabidhiwa fomu ya Uteuzi wa Ubunge na Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.