Na. Elinipa Lupembe.
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Arumeru Magharibi Saad Mtambule , amemkabidhi rasmi fomu za Uteuzi wa Ubunge Jimbo la Arumeru Magharibi, Bw. John Emmanuel Lairumbe wa chama cha Alliance for Change and Transarency (ACT- WAZALENDO ).
Mgombea huyo amewasili kwenye Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo, eneo la Sekei akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa Chama cha ACT-WAZALENDO mkoa wa Arusha, majira ya saa 08:23 mchana na kukabidhiwa fomu hizo za Uteuzi mnamo saa 08:29 mchana, akiwa ni mteule wa chama cha ACT-WAZALENDO, kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo.
Aidha Msimamizi huyo wa Uchaguzi, amemkabidhi fomu ya Uteuzi mgombea huyo, kufuatia Maelekezo ya Fomuya Uteuzi Na. 8B, kwa mujibu wa Kifungu cha 38 (3) na (4) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343 ikiweka wazi mambo yaliyojumuishwa kwenye fomu ya Uteuzi.
Hata hivyo Msimamizi Mtambule amemtaka mteule huyo, kusoma maelekezo yanayotolewa na Tume ya Taifa Ya Uchaguzi, sambamba na kuheshimu taratibu za uchaguzi kwa kufuata maelekezo hayo, maelekezo yatakayowezesha uchaguzi kuwa wa amani, huru na haki kwa manufaa ya watanzania wote .
Mgombea huyo amefanya idadi ya Wagombea kuwa tisa mpaka sasa, kutoka vyama tisa vya siasa, kuchukua fomu ya Uteuzi wa Ubunge kiwania Jimbo la Arumeru Magharibi.
PICHA ZA MATUKIO.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.