• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

NENDENI MKAPATE CHANJO, CHANJO YA UVIKO 19 NI SALAMA: DC ARUMERU MHANDISI RUYANGO

Posted on: August 3rd, 2021

Na. Elinipa Lupembe.

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mheshimwa Mhandisi Richard Ruyango, amewataka wananchi wilayani humo, kwenda kupata chanjo ya ugonjwa hatari duniani, unaosababishwa na virusi vya corona 19 (UVIKO 19), kutokana na ukweli kwamba chanjo hiyo ni salama na iimethibitishwa na watalamu wa afya kwa viwango vya kimataifa.

Mkuu huyo wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Ruyangwa ametoa rai hiyo wakati akizinduzi rasmi wa zoezi la chanjo ya ungonjwa wa virusi vya  Corona 19 ( UVIKO 19) katika halmashauri ya Arusha, zoezi lililofanyika kwenye hospitali ya wilaya  Olturumet na kuendelea kutolewa kwenye vituo vingine vitatu vilivyoainishwa katika halmashauri hiyo.

"Leo tumezindua chanjo ya UVIKO 19 katika wilaya yetu ya Arumeru, inayohusha wananchi wa halmashauri za Meru na Arusha, niwatake wananchi wangu, kutumia fursa hiyo iliyotolewa na serikali bila gharama yoyote licha ya kuwa serikali imetoa uhuru wa mtu kuamua kuchanja ama la, lakini ni vema kutambua kinga ni bora kuliko tiba" amefafanua Mkuu huyo wa Wilaya.

Hata hivyo, wananchi wa halmashauri ya Arusha, wamejitokeza kwa wingi katika hospitali hiyo kwa ajili ya kupata chanjo hiyo, bila kujali makundi matatu yaliyoanaishwa na serikali kuanza kuchanjwa, wakiwemo viongozi wa chama na serikali, viongozi wawakilishi wa  wananchi, waheshimiwa Madiwani, viongozi wa dini na mila pamoja na watu wa rika mbalimbali.

Naye Mwenyekiti  wa halmashauri ya Arusha na Diwani wa kata ya Laroi, mheshimiwa Ojung'u Salekwa, amewataka wananchi kutumia fursa hiyo adhimu iliyotolewa na serikali kwa kufanya maamuzi sahihi na kufika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya vilivyoainishwa na kuchanja chanjo hiyo, kwa kuwa imethibitishwa na watalamu wa afya kupitia shirika la afya duniani na wizara ya afya, licha ya kwamba chanjo hiyo ni hiari.

"Ninaipongeza serikali kupitia Wizara ya Afya, kwa kutuletea chanjo ya ugonjwa hatari wa Corona, mimi kama  kiongozi nimekuwa wa kwanza kuchanja katika halmashauri yangu, ili kuonyesha mfano kwa wananchi wangu, chanjo ni salama, hivyo wananchi wanatakiwa kuachana na maneno ya kwenye mitandao, watumie fursa iliyotolewa na serikali kuchanja, hata kama chanjo hiyo ni hiari "amesema Mheshimiwa Ojung'uNaye 

Mzee wa ukoo, Laigwanani Boniface Tarakwa, amewataka wananchi kuacha kusikiliza maelezo ya uzushi yanayotolewa kwenye mitandao ya kijamii, kwamba chanjo hiyo ina madhara mara baada ya kuchomwa, lakini maneno hayo hayana ukweli, kwa kuwa yeye amechanja na hajaona mabadiliko yoyote kimwili ni kama chanjo nyingine alizowahi kuchanja. 

"Mimi nimechanja leo sijaona mabadiliko yoyote, maneno ya kwenye mitandao yanawajengea hofu, tafuteni taarifa shaihi kutoka kwa watalamu  msikubali  kupotoshwa kama ni chanjo tumesha chanja chanjo nyingi, tunapaswa kufuata maagizo ya watalamu wa afya ili kujikinga na gonjwa hili hatari la corona" amesisitiza Mzee wa Mila

Naye Steven Laiza (59) anayefanya kazi za Utalii, amesema kuwa rais amefanya jambo jema na la hekima sana, Tanzania sio kisiwa, tunamchangamano na nchi nyingine duniani, hatuwezi kwenda tofauti na nchi za wenzetu, ni muhimu serikali kuhakikisha inaleta chanjo za kutosheleza wananchi wote.

Hata hivyo Mganga Mkuu, halamshauri ya arusha, Dkt. Petro Mboya, amesema kuwa halmshauri ya Arusha imepata jumla ya chanjo 11,082, na kuainisha makundi maalumu yatakayopata chanjo hizo ni pamoja na wahudumu wa afya, walimu, watu wenye magonjwa sugu yasio ambukiza, watu wenye umri mkubwa wa kuanzia miaka 50 na kuwahimiza wananchi kujitokeza kwenye vituo vya kutolea huduma za Afya, huku akibainisha vituo hivyo ni Hospitali ya Olturumet, Haospital ya Seliani Ngaramtoni, Kituo cha Afya Mduruma na Zahanati ya Ngorbob kata ya Matevesi eneo la Kisongo.

Aidha Dkt. Mboya amewasisitiza wananchi kuendelea kufuata maelekezo yanayotolewa na wahudumu wa afya kwa kunaa mikono kwa sabuni na maji tiririka, kutumia vitakasa mikono, kuvaa barako, kuepuka misongamano isiyo ya lazima.Awali uzinduzi huo, umefanyika kufuatia agizo la Serikali kupitia wizara ya Afya, la wananchi kupata chanjo hiyo ya UVIKO 19 katika mikoa yote ya Tanzania.


Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha, mheshimiwa Ojung'u Salekwa akichomwa sindano ya chanjo ya UVIKO 19, wakati wa zoezi la uzinduzi wa chanjo ya UVIKO 19, katika  halmashauri ya Arusha, kwenye hospital ya wilaya ya Olturumeti


Kaimu Mkurugenzi halmashauri ya Arusha, mwalimu Hossein Mghewa akichomwa sindano ya  chanjo ya UVIKO 19, wakati wa zoezi la uzinduzi wa chanjo ya UVIKO 19, katika  halmashauri ya Arusha, kwenye hospital ya wilaya ya Olturumet


Afisa Mipango halmashauri ya Arusha, Anna Urio akichomwa sindano ya  chanjo ya UVIKO 19, wakati wa zoezi la uzinduzi wa chanjo ya UVIKO 19, katika  halmashauri ya Arusha, kwenye hospital ya wilaya ya Olturumeti

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.