Na Elinipa Lupembe
Historia nyingine inandikwa tena shule ya sekondari Mringa, baada ya ujenzi wa vyumba vya madarasa serikali imetoa kutoa fedha kiasi cha shilingi milioni 360 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili na ukarabati wa bweni mne kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita.
Kiasi hicho cha fedha ni muendelezo wa mkakati wa serikali wa uboreshaji wa miundombinu ya shule nchini ili kuwa na mazingira bora, rafiki na wezeshi kwa walimu na wanafunzi katika tendo la kufundisha na kujifunza kwa shule za serikali nchini.
Mkurugenzi Mtendaji, halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, amesema kuwa milioni 360 zitatumika kujenga mabweni mawili yenye kulaza wanafunzi 80 kila moja na kukarabati mabweni maane ya zamani yenye kulaza wanafunzi 40 kila bweni na kufanya mabweni yote kulaza wanafunzi 320.
Aidha Mkurugenzi Msumi, ameishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuona umuhimu wa kujenga mabweni mara baada ya kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa, husani kwenye shule zenye wananfunzi wengi kama ilivyo Mringa, jambo ambalo linawapa fursa wanafunzi kuwa na mazingira bora pamoja na muda mrefu wa kujifunza na kufanya marudio kwa kujisomea muda wote wawapo shuleni.
"Fedha hizi zimekuja wakati muafaka, kutokana na uhitaji mkubwa wa mabweni ambayo licha ya kuwapa wanafunzi muda mrefu wa kujisomea zaidi unawapa walimu uwanda mpana wa kumudu hali ya ufundishaji na malezi kwa wanafunzi kipindi chote wawapo shule " Amesema Msumi
Naye Mkuu wa shule ya sekondari Mringa Mwl. Salum Magaka amebainisha umuhimu wa mabweni shuleni hapa, kutokana na uhitaji mkubwa wa wanafunzi kuishi shuleni jambo ambalo linawapa fursa walimu na wanafunzi kurahisisha tendo la kujifunza na kufundisha vinavyoendana na malezi kwa wanafunzi.
Uwepo wa mabweni unaiwezesha shule kuwa na ratiba zinazoenda hadi usiku na kuwafanya wanafunzi kuwa na muda mrefu wa kujisomea tofauti na mwanafunzi anayekwenda na kurudi shuleni kila siku kwa kuwa hupoteza muda mwingi njiani.
Ameitaja siri ya mafanikio na ufaulu wa juu shuleni hapo, hasa kwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita ni uwepo wa mabweni ambao unawapa nafasi wanafunzi kujisomea muda wote kutokana na ratiba za masomo kwend ahadi mida ya usiku.
"Mwanafunzi akiishi bweni anatawaliwa na ratiba 'fixed' ya shule, ipo ratiba ya kawaida ya siku, na ratiba ya kujisomea usiku ambayo humlazimu mwanafunzi kuifuata, tofauti na mwanafunzi anayeishi nyumbani ambapo hupoteza muda mwingi njiani na wengine kukosa muda wa kufanya marudio kutokana na kupewa majukumu na kazi nyingi za nyumbani". Amesema Mwl. Magaka
Shule ya sekondri Mringa ni miongoni mwa shule kongwe zinazofanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa yenye kidato cha I ampaka cha VI, ikuwa na jumla ya wanafunzi 1,962 wavulana 617 na wasichana 1,345 huku wanafunzi 375 ni wa kidato cha tano na cha sita.
ARUSHA DC NI YETU, TUSHIRIKIANE KUIJENGA
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.