Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam
OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, imeshika nafasi ya pili kati ya Wizara 10 bora kutoa habari kwa umma.
Tuzo hizo zilizokabidhiwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari zimetolewa kwenye Kongamano la kitaifa la maendeleo ya sekta ya habari lililofanyika leo jijini hapa.
Ofisi ya Rais TAMISEMI imeshika nafasi ya pili kutokana na kuchapisha habari nyingi na za kina kwenye vyombo vya habari, kuchapisha picha, kuwa na vipindi katika redio na televisheni pamoja na matumizi bora ya mitandao ya kijamii.
Mbali na Ofisi ya Rais-TAMISEMI, nafasi ya kwanza imechukuliwa na Wizara ya Afya, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Wizara ya Maliasili na utalii, wizara ya mambo ya ndani ya nchi, wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Pia wizara ya Kilimo, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wazee na Mkundi Maalum, Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Pia Ofisi ya Rais TAMISEMI imetoa Tuzo Kwa Mwandishi wa magazeti ya Serikali Anastazia Anyimike Mwaipyana kutokana na mchango katika kutoa habari za wizara hiyo.
Akizungumzia Tuzo hiyo, Bi. Anastazia alisema:" nashukuru sana TAMISEMI kwa kuniheshimisha. Niwaahidi kuendelea kushirikiana na Wizara katika kuhabarisha umma katika masuala mbalimbali ikiwemo na kazi kubwa inayofanywa Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Ofisi yake ya TAMISEMI kujulisha umma miradi inayotekelezwa inayokwenda kuwanufaisha wananchi."
Pia Ofisi ya Rais TAMISEMI imempatia Mhariri na Mtangazaji wa Milard Ayo Tv Bakari Chijuba kwa kazi kubwa aliyofanya katika kutangaza kazi za Ofisi ya Rais-TAMISEMI.
Na kupitia taasisi yake ya Wakala wa Barabara za mijini na Vijijini(TARURA) wamempatia Tuzo Shabani Omari matwebe ambaye ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanahabari Mitandao ya Kijamii Tanzania ambaye pia ametoa mchango mkubwa katika kutangaza kazi za Wakala huyo.
Kongamano hili ni la kwanza kufanyika nchini na litaendelea kufanyika kila mwaka na kukutanisha Maafisa habari, waandiahi wa habari na wadau wa habari kujadili maendeleo ya sekta ya habari nchabar
KaziInaenKaziInaa✍
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.