• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

PSSSF YATETA NA WATUMISHI ARUSHA DC KUHUSU KIKOKOTOO

Posted on: October 6th, 2022

Na Elinipa Lupembe 


Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma  (PSSSF), wamekutana na watumishi wa Makao Makuu,  halmashauri ya Arusha, kwa lengo la kukumbushana  majukumu na wajibu wa mfuko kwa watumishi pamoja na mabadiliko ya mfuko, ikiwemo kikokotoo cha mafao ya kustaafu.

Akizungumza kwenye kikao kazi hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo, Afisa Mwandamizi PSSSF Kanda ya Kaskazini, Venance Mwaijibe, amesema kuwa, Mfuko wa PSSSF una jukumu la kuwahudumia watumishi wa Umma  hivyo watumishi wanapaswa kuufahamu mfuko na huduma wanazostahili kupata wakiwa kwenye ajira na sio mpaka kustafu.

Mwaijibe ambainisha kuwa watumishi wengi hufika ofisi za PSSSF pindi wanapolazimika kuanza kufuatilia mafao ya kustaafu, jambo ambalo si sahihi, mtumishi anatakiwa kufika na kuufahamu mfuko mara anapoanza makato na kuendelea kufuatilia mpaka pale anapofikia muda wa kustaafu.

Aidha ameyataja mafao yanayotolewa na mfuko ni pamoja na uzee, uzazi, ugonjwa, ulemavu, kukosa ajira na warithi, na kufafanua kuwa baadhi ya mafao si lazima mtumishi awe amestaafu utumishi wa Umma.

Aidha ametoa ufafanuzi wa maana halisi ya kikokotoo cha asilimia 33 na kufafanua kuwa, kuanzia tarehe 01 Julai, 2022, mtumishi atakapostaafu atapatiwa fao la mkupuo la asilimia 33 na kuendela kupata fedha kwa mwezi kipindi chote cha maisha yake kwa kuzingatia kanuni za kikokotoo cha hesabu za mfuko.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji, amelishukuru shirika hilo kwa elimu waliyoitoa kwa watumishi, elimu ambayo imefungua wigo na uelewa mpana wa kufahamu wajibu wa mwajiri na haki za mtumishi, elimu ambayo inapaswa kutolewa mara kwa mara kwa watumishi ili kuondoa sintofahamu kwa watumishi walio wengi.

"Tumeleweshwa manufaa ya mfuko kwa watumishi pindi watakapostaa, na kuondoa dhana potofu iliyojengeka kwa watumishi wengi na kuuona mfuko kama ni unyonyaji jambo ambalo si sahihi, elimu hii ni muhimu na inapaswa kutolewa kwa watumishi mara kwa mara". Amesisitiza Msumi

Naye Mwanasheria wa Halmashauri ya Arusha, Mhudini Lesirwa, ameomba marekebisho ya sheria ya fao la uzazi kupatiwa wanaume pindi wenza wao, wanapojifungua kwa kuwa, wapo wanaume ambao ni watumishi lakini wenza wao si watumishi.

"Mfuko unapaswa kufikiria kutoa fao la uzazi kwa wanaume ambao wenza wao si watumishi, ili nao wafaidi mfuko huo sawa na wanawake, kwa kuzingatia kila mwanachama ana haki sawa bila kuzingatia jinsi yake". Ameweka wazi Lesirwa

Kikao kazi hicho, kimetoa nafasi kwa watumishi kuuliza maswali mengi na kupatiwa majibu, jambo ambalo limejenga uelewa wa pamoja kati ya wwatumishi na Mfuko hususani kwenye suala zima la kikokotoo.


ARUSHA DC

KaziInaendelea

PICHA ZA MATUKIO WAKATI WA KIKAO KAZI



 Afisa Mwandamizi PSSSF Kanda ya Kaskazini, Venance Mwaijibe, akizungumza na watumishi wa Makao Makuu halmashauri ya Arusha, kwenye kikao kazi cha kujadili masuala mbalimbali ya Mfuko wa PSSSF, kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo.


Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Arusha Seleman Msumi, akizungumza na watumishi wa Makao Makuu halmashauri ya Arusha, kwenye kikao kazi cha kujadili masuala mbalimbali ya Mfuko wa PSSSF, kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo.




Baadhi ya watumishi wa makao makuu halmashauri ya Arusha wakifuatilia mijadala juu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii PSSF wakati wa kikao kazi cha kujadili masuala mbalimbali ya Mfuko wa PSSSF, kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo.












Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.