Hatimaye kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Sahili Nyanzabara Geraruma amekabidhi Mwenge wa Uhuru Salama Kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Samia Suluhu Hassan, katika sherehe za kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na kumbukizi ya baba wa Taifa Oktoba 14 kwenye uwanja wa Kaitaba Mkoani Kagera.
Katika taarifa ya Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge, amebainisha kuwa Mwenge wa Uhuru mwaka 2022 umekimbizwa katika mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani na kupitia jumla ya Miradi 1,263 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 650.
Hata hivyo kiongozi huyo amebainisha kuwa katika kutembelea miradi hiyi Mwenge wa Uhuru ulikataa kuzindua na kuweka mawe ya Msingi kwenye Miraidi 65 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 12 iliyogubikwa na dosari ikiwemo Rushwa, Uzembe na Ubadhirifu.
Aidha Mheshimiwa Rais ametoa maelekzo kwa taasisi za kuzui na kupambana na rushwa TAKUKURU na ZAECA kufanya Uchunguzi na kuchukuwa hatua stahiki kwa wote waliobainika kufanya ubadhirifu wa fedha za umma kwenye Miradi hiyo 65 iliyokataliwa na Mwenge mara baada ya kubainika kuwa na dosari ikiwemo Rushwa Uzembe na Ubadhirifu.
Pamoja na hayo Rais Samia ametoa wito kwa Watanzania kuyaenzi Mema na Mazuri tuliyoachiwa na hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikiwemo kuikataa Rushwa, Uzembe na Ubadhirifu wa fedha za umma.
Hata hivyo Rais Samia amewapongeza Viongozi wa Mbio za Mwenge kwa uaminifu na uzalendo mkubwa walioonyesha ikiwa ni pamoja na kuikataa miradi yenye Mashaka na dosari.
Ikumbukwe kuwa Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2022 umekimbizwa kwa siku 195 kwenye Halmashauri 195 na kuweka mawe ya Msingi na kuzindua Miradi 1,263 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 650 Chini ya wakimbiza Mwenge 6.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.