• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RAS ARUSHA AWASIHI WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO KAMA TIMU

Posted on: October 21st, 2022

Na Elinipa Lupembe


Katibu Tawala mkoa wa Arusha, Missaile Musa, amewataka watumishi kufanya kazi kwa weledi kwa kushirikiana pamoja kama timu, ili kufikia lengo la halmashauri na serikali kwa ujumla la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Katibu Tawala huyo, ametoa rai hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi katika halmashauri ya Arusha na kupata fursa ya kuzungumza na watumishi wa Makao Makuu,  ikiwa na lengo la kukumbushana namna bora ya utekelezaji wa majukumu kwa watumishi wa Umma.

Katibu Tawala Missaile ameweka wazi kuwa licha ya kuridhishwa na kazi nzuri inayofanywa na watumishi wa halmashauri hiyo na kuufanya mkoa wa Arusha kuwa miongoni mwa mikoa inayofanya vizuri nchini, amewasisitiza kuendelea kuwajibika ipasavyo bila kukata tamaa.

Aidha amebainisha kuwa licha ya changamoto zinazojitokeza kukwamisha utekelezaji wa majukumu, amewahimiza kutumia rasilimali zilizopo na kuendelea kishirikiana kama timu moja, kuhakikisha wananchi wa mkoa wa Arusha wanapata huduma kupitia wao kama ilivyo lengo la serikali.

"Nafahamu kuna changamoto nyingi lakini zisitukwamishe wala kutukatisha tamaa, tuzigeuze kuwa fursa, niwasisitize   kila mmoja kutimiza wajibu wake kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za utumishi wa Umma, tumieni taaluma zenu kwa kushirikiana kwa sekta zote kwa kuwa kila sekta zote inategemea sekta nyingine" Amesisitiza Maiselle

Hata hivyo watumishi halmashauri ya Arusha, wamepata fursa ya kuelezea changamoto zinazowakabili, katika kutimiza majukumu yao, na kumuamba katibu Tawala kushughulikia zile zilizo ndani ya uwezo wake jambo ambalo litaongeza ari ya wawatumishinkufanya kazi.

Naye Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango, amemshukuru katibu Tawala huyo na kuahidi kutekeleza maagizo yote ikiwa ni pamoja na kuwasimamia watumishi kutekelza majukumu yao kwa weledi kwa kuzingatia taratibu za utumishi wa Umma.

"Watumishi hawa wanapambana sana kuhakikisha huduma kwa wananchi zinapatikana na zaidi tunamshukuru Rais wetu mama Samia Suluhu kwa kuboresha maslahi ya watumishi, ikiwemo kupandishwa kwa madaraja kwa watumishi wote ambao walikuwa wanastahili, nikuahidi hatutamuangusha mheshimiwa Rais". Amebainisha Mhandisi Ruyango

Awali katika ziara hiyo, licha ya kuzungumza na watumishi, katibu Tawala ametembelea miradi mimnee ya maendeleo katika sekta ya afya, elimu na miundombinu ya barabara.


ARUSHA DC

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.