Na Elinipa Lupembe
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella amekemea tabia ya wananchi wa kata ya Oldonyowas kuchoma shule, mchezo ambao unajirudiaridia kwa shule ya sekondari Oldonyowas kuchomwa.
Akizungumza na wananchi wa Kata ya Oldonyowas na Oldonyosambu, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya soko la Oldonyosambu, amewataka wananchi hao kuacha mara moja tabia inayyojirudia ya kuchoma shule ya sekondari Oldonyawas
Mhe. Mongella ameweka wazi kuwa uchomaji wa shule hiyo umekuwa, wanazo taarifai za ndafni vitendo hivyo hufanywa na watu wa eneo hilo, huku akiwatuhumu wananchi hao, kuwafahamu wahalifu hao na kuwaficha.
"Tunazo taarifa za kiintelijensia wanaochoma shule ni wakazi wa hapahapa na mnawafahamu, tabia hii ikijirudia serikali itachukua hatua kali dhidi yenu, kwa kuanza na viongozi wa maeneo haya, wacheni kabisa tabia hiyo
Aidha amemtaka Diwani wa Kata ya Oldonyowas Kijana Saruni kwa kushirikiana na wenyeviti wa vijiji na vitongoji, kuhakikisha tabia hiyo ya uchomaji wa shule inakoma mara moja kwa kuwa licha ya kuiingizia Serikali hasara na gharama kubwa ya ukarabati pasipo ulazima lakini zaidi inahatrisha maisha ya watoto wasio na hatia.
"Tunazo taarifa za watu wanaofanya vitendo hivyo viovu kutokea kwenye maeneo yenu na mnawafahamu, viongozi wa kata na vijiji, shirikianeni kudhibiti tabia hiyo mbali, na niwaahidi ikitokea tena serikali haitawaacha salama kijiji kizima" Amesema
Sambamba na kusikiliza kero za wananchi Mhe. Mongella amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya Elimu, Maji na miundombinu ya Barabara.
Hata hiyo, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha, kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati na kwa viwango vya ubora unaotakiwa kulingana na thamani ya fedha zilizotolewa na Serikali.
Sekei Road
Anuani ya posta: 2330 Arusha
Simu : +255 027 2502737
Simu: 073 65000476
Barua pepe: ded@arushadc.go.tz
Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.