• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RUZUKU YA TASAF YAWEZESHA KAYA KUPATA MITAJI YA BIASHARA NDOGONDOGO

Posted on: October 4th, 2022

Na Elinipa Lupembe

Fedha za ruzuku zinazotolewa na serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii - TASAF na mpango wa Kunusuru Kaya Masikini, zimeanza kuzaa matunda kwa kuwawezesha wanufaika wa mpango huo, kuanzisha biashara ndogo ndogo na kujikimu na hali ngumu ya maisha.

Wanufaika hao, wamekutwa na mwandishi wetu, wakiwa kwenye biashara ya nguo za mitumba, wakati wa kupokea ruzuku ya fedha za ruzuku kwa mwezi wa 7/8 mwaka 2022, kwenye ofisi ya Kijiji cha Laroi kata ya Laroi, halmashauri ya Arusha, wilaya ya Arumeru.

Aidha wanufaika hao wameelezea hisia zao kwa serikali kupitia TASAF, namna imezitoa kaya hizo kwenye hali ngumu ya kiuchumi ya kushindwa kumudu hata kupata mahitaji ya lazima kwa familia zao, na kuongeza kuwa kwa sasa wameanza kusahau mateso hayo.

"Tunamshukuru Mungu, tunamshukuru Mama Samia, ameleta neema kwa kina mama, amekuwa ni mfano kwa kina mama, kila mama anajiamini kupitia Mama Samia, kama Rais anafanya kazi kwa nini sisi tusifanye, hakuna mwanamke analala siku hizi, TASAF imetutoa gizani". Wameweka wazi  kina mama hao

Zaina Ebeneza (32) mnufaika wa TASAF kijiji cha Laroi na mama wa watoto watano, amebainisha kuwa amekuwa akopokea ruzuku ya shilingi 54,000, fedha iliyomuinua kutoka kwenye lindi la umaskini uliokithiti na kumuwezesha kupata mtaji wa kuuza nguo za mitumba.

"Ninauza nguo kwa kutembeza lakini pia ninauza kwenye minada siku ya soko, TASAF imenitoa mbali sana, nilikuwa na hali ngumu sana kimaisha,  nina watoto watano wananitegemea,  kwa sasa hali yangu imeimarika, ninafanya biashara yangu na ninapata mahitaji ya familia, watoto wanasoma na kupata mahitaji yao kama watoto wengine". Amesema Zaina

Naye Ester Lobulu ( 50) mfanyabiashara wa nguo na mbogamboga, amesema kuwa analea watoto na wajukuu watatu, mmoja ni yatima, ruzuku ya TASAF imemsaidia kufanya biashara nguo, siku za soko la Mirongo, nasiku za kawaida huuza mboga kwa kutembeza majumbani.

"Tunamshukuru Mungu, tunamshukuru mama Samia, TASAF imetusaidia hasa wamama, tulikuwa tunateseka na maelezi ya familia, mume aliniacha na akaniachia watoto, ninawasomesha, maisha sio magumu sana kwa sasa ninapambana na Mungu ananisaidia, siku za mnada nauza nguo Mirongoine, siku za kawaida natembeza mboga kwenye nyumba za watu". Amesema Ester.

Ifahamike kuwa Mpango wa kunusuru kaya masikini unalenga kuziwezesha kaya kuondokana na umasikini uliokithiri kwa kupambana na adui ujinga, umasikini na maradhi kupitia ruzuku ya msingi ya kuiwezesha kaya kupata mahitaji ya chakula na mavazi, ruzuku ya elimu ya kuhakikisha watoto wa kaya wa kuanzia miaka 7- 18 wanapata elimu ya msingi huku watoto wa miaka 0-5 wanapata huduma za afya kwa kuhudhuria kliniki nankupata chanjo kwa kipindi chote.


ARUSHA DC

KaziInaendelea✍✍

PICHA ZA WALENGWA WAKIWA KWENYE BIASHARA ZAO


Ester Lobulu (50) mnufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya masiikini, wa kijiji cha Laroi kata ya Laroi akiwa kwenye biashara yake ya kuuza nguo mtaji ambao amekiri kuupata kutokana nanfedha za ruzuku anayopikea kutoka TASAF.





Ester Lobulu (50) mnufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya masiikini, wa kijiji cha Laroi kata ya Laroi akiwa kwenye biashara yake ya kuuza nguo mtaji ambao amekiri kuupata kutokana nanfedha za ruzuku anayopikea kutoka TASAF.






Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA ENABOISHU FM - ARUSHA DC May 26, 2025
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya

  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA CHAKULA BORA

    May 28, 2025
  • VIONGOZI WA DINI WAPEWA ELIMU YA AFYA YA MAMA NA MTOTO

    May 27, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI YA MKATABA

    May 26, 2025
  • RC MAKONDA ATEMBELEA NA KUKAGUA MRADI WA UJENZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA ARUSHA

    May 25, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.