• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe |
Arusha District Council
Arusha District Council

Serikali ya jamuhuri ya Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili Makuu
    • Mikkati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara na Vitengo
      • Utawala na Utumishi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Fadha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maji
      • Works
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo na Umwagiliaji na Ushirika
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
      • UKIMWI/ AIDS
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Livestock
    • Wadau wa Maendeleo
  • Huduma Zetu
    • Health
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Utawala Fedha na Mipango
      • Elimu Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Vikao vya Timu ya Uendeshji ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mktaba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa UMMA
    • Video za Shoghuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali ya Japani yawekeza kutokomeza vifo vya mama na mtoto Mlangarini

Posted on: April 9th, 2019

Na. Elinipa Lupembe.

Kufuatia uhusiano mzuri ya kirafiki, yaliyojengeka kati ya Tanzania na serikali ya watu wa Japani, Japani kupitia ubalozi wake nchini Tanzania, imeunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano, kwa kuchangia fedha kiasi cha shilingi milioni 191 na kukamilisha, ujenzi wa kituo cha kisasa cha Afya cha Manyire kata ya Mlangarini, halmashauri ya Arusha wilaya ya Arumeru.

Ubalozi huo wa Japani umefikia hatua hiyo,  baada kuridhishwa sera ya serikali ya kukabiliana na changamoto za huduma za afya, na kuamua kuwasaidia wananchi wa kata ya Mlangarini na vitongiji vyake, kuwaondolea  na adha ya kutembea umbali wa zaidi ya Kilomita 40 kwenda kupata huduma za afya kwenye hospitali ya mkoa ya Mount Meru.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho cha Afya, Balozi wa Japani nchini, Balozi Shininchi Goto, amesema kuwa, serikali ya Japani iligundua adha ya upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Mlangarini,  ya kukosa huduma za afya katika maeneo yao,  na kuamua kuwasaidia kumalizia ujenzi wa kituo chao cha afya, ambacho tayari walikuwa wameanza na kukwama kwa muda.

Balozi huyo amethibitisha kuwa, ukosefu wa huduma za afya karibu,  ilikuwa ni hatari hasa kwa kina mama wajawazito na watoto, ambao baadhi yao walipoteza maisha kwa kuchelewa kupata matibabu, kulikosababishwa na umbali wa hospitali, huku akiamini kituo hicho cha afya kitaokoa maisha ya watu wengi tofauti na hapo awali.

"Serikali ya Japani imeamua kusaidia kuokoa maisha ya watu vinavyotokana na vifo visivyo vya lazima, vinavyotokana na kuchelewa kupata huduma, ninategemea mtakitunza kituo hiki ili kiweze kuwahudumia kwa muda mrefu" amesema Balozi  Goto.

Mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro, licha ya kuishukuru serikali ya Japani, amesema kuwa msaada huo umetokana na mahusiano mema ya serikali na nchi ya Japani, yaliyojikita kwenye sera imara za serikali ya awamu ya tano ya kuboresha huduma za afya, kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma za msingi katika maeneo yao.

Ameongeza kuwa, uwepo wa kituo hicho cha Afya, utasaidia  kutokomeza vifo vya wanawake na watoto, vilivyotokana na ukosefu wa huduma za haraka kwa wagonjwa na akifafanua kuwa, kwa sasa Kata ya Mlangarini imetekeleza adma ya serikali kwa asilimia 100, kwa kuwa na zahanati kwenye vijiji vyake vyote na kituo cha afya.

Hata hivyo, mwanzilishi wa ujenzi wa kituo hicho cha Afya, Diwani mstaafu wa kata ya Mlangarini, Mathias Manga ameshukuru serikali ya Japani, na amethibitisha kuwa na mkakati wa kutafuta fedha, kiasi cha shilingi milioni 150, kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za madaktari na wauguzi, ili wananchi hao waweze kupata huduma kwa muda wote.

Naye Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya Arusha, Dkt. Wilson Mahera, ameshukuru Ubalozi huo wa Japani na kufafanua kuwa, kituo hicho cha afya ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo na  kinategemea kutoa huduma kwa zaidi ya watu 6,000 wa kata ya Mlangarini na vijiji vya kata jirani ya Bwawani, kata ambayo mpaka sasa haina kituo cha afya.

Ujenzi wa kituo hicho cha Afya, ulianza mwaka 2013 na kusimama kwa muda mrefu kutokana na ukosefu wa fedha, mwaka 2017 ndipo ubalozi wa Japani ulipoanza ujenzi na umekamilika kwa gharima ya shilingi milioni 468.6, huku shilingi milioni 120, Diwani Mathias Manga, milioni 20 nguvu za wananchi, milioni 83, serikali kupitia mapato ya ndani na ubalozi wa Japani milioni 191.


Balozi wa Japani nchini Tanzania, Balozi Shinichi Goto akikata utepe kuzindua kituo cha Afya Manyire kata ya Mlangarini.

Balozi wa Japani nchini Tanzania, Balozi Shinichi Goto akipiga makofi mara baada ya kukata utepe na kuzindua kituo cha Afya Manyire kata ya Mlangarini.


Balozi wa Japani nchini Tanzania, Balozi Shinichi Goto, akizungumza na mkuu wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro  mara baada ya kuzinduliwa kwa kituo cha Afya Manyire kata ya Mlangari



Muonekano wa nyuma wa jengo la kituo cha Afya Manyire

Matangazo

  • MTIHANI WA DARASA LA SABA 11-12/09/2024 September 09, 2024
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2023 ARUSHA DC June 11, 2023
  • ZIARA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAMISEMI, MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA 17 SEPTEMBA 2024 September 13, 2024
  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI WA ROBO YA TATU 2O21/2022 tarehe 09.05.2022 May 08, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya

  • MKURUGENZI WA ARUSHA DC,BW.SELEMAN MSUMI AKIWA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI HIYO KATIKA MASDHIMISHO YA MEI MOSI KIMKOA ARUSHA

    May 02, 2025
  • HERI YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • HERI YA SIKU YA MEI MOSI

    May 01, 2025
  • MHE. MAJALIWA MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI

    April 29, 2025
  • Tazama zote

Video

Video zaidi

Viunganishi vinavyoingiliana

  • Leseni ya vileo
  • Fomu ya ukaguzi

Viunganishi vinavyohusiana

  • Tovuti kuu ya serikali
  • Tamisemi
  • Utumishi portal
  • Wakala wa serikali mtandao
  • Mkoa wa arusha
  • ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Sekei Road

    Anuani ya posta: 2330 Arusha

    Simu : +255 027 2502737

    Simu: 073 65000476

    Barua pepe: ded@arushadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2018 Arushadc . All rights reserved.